Serikali Mpanda yafunga kijiji, yahamisha waliovamia hifadhi ya msitu

Na Walter Mguluchuma-Mpanda Serikali ya wilaya ya Mpanda imetangaza kuwahamisha wananchi wote wanaoishi katika Kitongoji cha Kamama Kat... thumbnail 1 summary
Na Walter Mguluchuma-Mpanda

Serikali ya wilaya ya Mpanda imetangaza kuwahamisha wananchi wote wanaoishi katika Kitongoji cha Kamama Kata ya Mpandandogo na kukifunga kijiji cha bugwe kilichopo katika Tarafa ya Kabungu wilayani hapa kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira.

Uharibifu huo unaofanywa na wafugaji na shughuli za kilimo na kusababisha uharibifu mkubwa wa msitu wa katuma ambao ndio chanzo kikuu cha mito mingi katika ukanda wa ziwa Tanganyika

Kauli hiyo imetolewa hapo juzi na mkuu wa wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake

Mwamlima alisema zoezi hilo la kuwahamisha watu waliovamia mistu hiyo  limeanza hapo septemba 14 na litadumu kwa muda wa siku kumi na nne  na linawashirikisha Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya, watumishi kutoka ofisi ya   Ardhi na Maliasili pamoja na Viongozi wa Vijiji husika.

Alifafanua kuwa uongozi wa Serikali ya Wilaya ya Mpanda umeamua  kuwahamisha wananchi wa Kitongoji Kamama kutokana   watu hao kuvamia  msitu unaotenganisha Kata ya Mpanda Ndogo na  makazi ya wakimbizi ya Mishamo eneo ambalo lilikuwa limetengwa kwa ajiri ya shughuli za uwekezaji

Alisema eneo hilo lenye jumla ya hekari 46,000 pia lilikuwa limetengwa kwa ajiri ya ujenzi wa kambi ya jeshi la kujenga Taifa na Shughuli za kilimo kwa vikundi vya vijana
Alieleza kuwa zoezi hilo la kuwahamisha watu hao litafanyika kwa kuwaelimisha kwanza wananchi hao ili waweze kutambua umuhimu wa misitu na tayari eneo la kuwahamishia limeisha andaliwa katika kijiji cha jirani kinanacha itwa Vikonge katika kata ya Mpanda Ndogo

Kwa upande wa Kijii cha Bugwe Mwamlima alisema uongozi wa Wilaya unawasiliana na ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili iweze kutowa kibali cha kukifunga kijiji hicho kwani Wizara hiyo ndio yenye mamlaka ya kukifunga au Kukifunga Vijiji hapa Nchini

Alifafanua kuwa kKjiji hicho ndicho kinachozungukwa na msitu ambao  ndio chanzo cha mito yote muhimu iliyoko  katika ukanda wa Ziwa Tanganyika  ambapo mito mingi imeanza kukauka kutokana na shughuli  zinazofanywa za kibinadamu

Uharibifu huo wa msitu wa Bugwe tayari umeisha anza kuathiri wanyama katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi  kutokana na kukauka kwa mto Katuma unao peleka maii katika mto wa Sitalike ulioko katika hifadhi ya Katavi kukauka na kusababisha vifo vya Mamba na Viboko  ambapo chanzo cha mto huo ni msitu wa Bugwe


Alisema kutokana na hari hiyo uongozo wa Wilaya umeamua kuinusuru hari hiyo na kuanzia sasa maeneo yote  ya Hifadhi ya misitu yatawekewa mabango yanayo kataza  watu kufanya shughuli za kibinadamu  katika misitu