Swissport yajipanga kiusalama

MENEJA wa Kampuni ya kuhudumia ndege, abiria na mizigo katika viwanja vya ndege (Swissport), Gaudence Temu, amesema wamejipanga kiusalama m... thumbnail 1 summary
MENEJA wa Kampuni ya kuhudumia ndege, abiria na mizigo katika viwanja vya ndege (Swissport), Gaudence Temu, amesema wamejipanga kiusalama muda wote ili kuzuia matukio mbalimbali ya kigaidi yasitokee kwenye viwanja vya ndege wanavyotoa huduma.

Temu alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana alipozungumza na Tanzania Daima juu ya maendeleo ya kampuni yake kwa kipindi cha miezi sita.

Alisema kwa kushirikiana na maofisa usalama wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege wanahakikisha usalama unakuwepo kwa abiria wao kwa kipindi chote.

Katika hatua nyingine, alisema wanakabiliwa na changamoto kubwa ya miundombinu kutokana na abiria na ndege kuongezeka na miundombinu ya viwanja hivyo kuendelea kuwa ya zamani.

Hata hivyo, aliishukuru serikali kwa kuendelea na ujenzi wa Terminal III, hivyo anaamini usumbufu huo utakwisha.


Chanzo: Tanzania Daima