Video: Mwindaji wa kizungu aua tembo na kujisifu kwenye kipindi cha TV

Shirika la habari la NBC limejikuta katika lawama nzito baada ya kurusha kipindi kinachoonyesha namna wawindaji wa wanyama wanavyoua wanyam... thumbnail 1 summary
Shirika la habari la NBC limejikuta katika lawama nzito baada ya kurusha kipindi kinachoonyesha namna wawindaji wa wanyama wanavyoua wanyama huku wakifurahia na kujipngeza kwa kunywa pombe kwa kufanya mauaji hayo.
Katika kipindi hicho kinachoitwa Under Wild Skies, Tony Makris kutoka National Rifle Association anaweka wazi namna anavyofurahia kuua wanyama maneo ambayo yameambatana na vitendo vya kumuua tembo kwa kumpiga risasi kisha kupiga nae picha na baadae kufungua shampeni kujipongeza.
Kitendo hiki kimewakera wengi na hakika kinapaswa kupigwa marufuku kama nia ya dhadi ya kupambana na mauaji ya wanyama Afrika imekusudiwa.

Tazama video ya kipindi chenyewe ambayo imewekwa na geographic

Wakati Afrika ikiwa katika hatari ya kupoteza tembo wake lakini vitendo kama hivyo vya kuuza tembo kwa kuwafurahisha wachache vinaendelea kushamiri, katika kipindi cha nyuma niliwahi kuleta makala iliyoonyesha wazungu wakiwa wameua twiga ili wapige nae picha tu kitu ambacho si cha kiungwana hata kidogo.