Madaraka Nyerere apanda tena Mlima Kilimanjaro kuchangisha pesa za ujenzi wa shule ya Kichalikani, Tanga

Ndiyo kwanza nimemaliza kukwea Mlima Kilimanjaro katika mwaka wa 6 wa  The Mwalimu Nyerere/Mt. Kilimanjaro Charity Climb  kuchangisha pesa... thumbnail 1 summary

Ndiyo kwanza nimemaliza kukwea Mlima Kilimanjaro katika mwaka wa 6 wa The Mwalimu Nyerere/Mt. Kilimanjaro Charity Climb kuchangisha pesa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa shule iliyopo kwenye kijiji cha Kichalikani, wilayani Mkinga, mkoa wa Tanga.

Pamoja nami katika msafara wa Mlima Kilimanjaro alikuwa E. Gassana. Tulifika kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro asubuhi ya tarehe 5 Oktoba, saa 2:30 asubuhi.

Kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro, mita 5,895 juu ya usawa wa bahari na sehemu iliyo juu kuliko zote katika bara la Afrika, kutoka kushoto: Pius Yahoo, muongozaji wetu; E. Gassana; mwandishi wa blogu hii; na Musa Juma, muongozaji msaidizi.

Wakazi wa kijiji cha Kichalikani walianza ujenzi wa shule mwaka 2009 kwa kutumia sehemu ya ushuru uliokusanywa kwenye soko la samaki. Baada ya kuona jitihada hizi, Saidi Masimango, aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia na Habari ya Shirika la Hifadhi ya Jamii alichangia shilingi milioni moja. Masimango alifariki mwezi Julai 2013.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Nurdin Babu, naye alichanga mabati 33, wakati Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza alitoa mabati 100.

Kiasi cha shilingi milioni 7 zinahitajika kumalizia kazi za ujenzi ambazo hazijakamilika pamoja na kununua madawati.

Tafadhali changa kwa njia zifuatazo:

Jina la Akaunti: Kijiji cha Kichalikani
Benki: National Microfinance Bank
Namba ya Akaunti: 4193300163
Tawi: Mkwakwani, Tanga.

Wanaochangia wanaombwa kutuma majina kamili na viwango vilivyotolewa (kwa madhumuni ya kuchapisha orodha kamili kwenye gazeti la Jamhuri) kwa:  madaraka.nyerere@gmail.com


Hata wasiopenda majina yao yachapishwe nao wanaombwa kuwasilisha hizo taarifa kwa njia hiyo ya barua pepe (majina hayatachapishwa).

Kuchangia kwa njia ya simu tumia namba ifuatayo (pesa zitakusanywa na kuwekwa kwenye akaunti ya benki iliyotajwa juu): +255 755 570 795