MAFUNZO KWA WATAALAM KUHUSU KEMIKALI ZINAZODUMU KATIKA MAZINGIRA KWA MUDA MREFU (POPs)

Bi Magdalena Mtenga, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais akimkaribisha mgeni rasmi kuf... thumbnail 1 summary
Bi Magdalena Mtenga, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais akimkaribisha mgeni rasmi kufungua mafuzo ya siku mbili ya wataalam wa mazigira Jijini Dar es Salaam kuhusu kemikali zinazokaa ardhii kwa muda mrefu,wataalaam hao washiriki wanatoka katika mkoa wa Dar es saala, Pwani na Zanzibar.
Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt Julius Ningu, akifungua mafunzo ya siku mbili wataaalam kutoka mkoa wa Dar es Salaam, Pwani na Morogoro, yanayohusu kemikali zinazokaa ardhini kwa muda mrefu, aliyekaa kushoto ni muwezeshaji kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Uhandisi Kemikali na Madini, Profesa Jamidu Katima.
Washiriki na wataalam katika mafunzo yanayohusu kemikali zinazokaa ardhini kwa muda mrefu katika mafunzo jijini Dar, wakimsikiliza mgeni Rasmi wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Picha ya Pamoja ya washiriki wa mafunzo ya wataalam,kuhusu kemikali zinazokaa ardhini kwa muda mrefu,Jijini Dar es Salaam leo. Habari na picha zote na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya Makamu wa Rais
Imeelezwa kuwa, kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya pembejeo, madawa ya matibabu na matumizi ya kemikali za viwandani hapa nchini, kumekuwa na ongezeko la hatari inayotokana na madhara kwa afya za binadamu, mazingira na viumbe hai yanayosababishwa na kemikali zinazodumu kwenye mazingira kwa muda mrefu.
Hayo yameelezwa leo katika ufunguzi wa mafunzo ya waataalam wa mazingira na usimamizi wa matumizi ya kemikali mbalimbali, jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi msaidizi wa idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bi Magdalena Mtenga.
Bi Magdalena ameeleza kuwa, Mlundikano wa madawa chakavu ya kilimo na matumizi mabaya ya madawa ya kilimo katika baadhi ya mikoa pamoja na shughuli za uzalishaji viwandani hapa nchini unachangia pia ongezeko la hatari hii.
Aidha Bi Magdalena aliongeza kwa kusema kuwa washiriki watawezeshwa kwa kutumia muongozo ulioandaliwa na UNIDO na FAO kuongeza elimu na uwezo wa kusimamia kemikali zilizo chini ya Mkataba wa Stockholm na kuepusha madhara ya kiafya na mazingira yatokanayo na kemikali hizi.
Awali akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Idara ya mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Julius Ningu, alisema kuwa, warsha hii ya mafunzo itakuza kuza uwezo wa wataalam hawa kwa lengo la kuwawezesha kusimamia kikamilifu kemikali aina POPs zilizoainishwa katika Mkataba wa Stockholm kwa mustakbali wa afya ya viumbe hai na ubora wa mazingira ikiwa ni pamoja na kutambua madhara mbalimbali yatokanayo na kemikali hizi pale ambapo zinatumika visivyo na kusababisha kuingia kwenye mfumo wa chakula na katika mazingira.
"Iwapo malengo haya yatafikiwa kupitia mafunzo haya, tutafanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa madhara yanayotokana na matumizi ya kemikali hizi na hivyo kufikia malengo makuu ya Mkataba. Alisisitiza"
Warsha hii ya mafunzo inashirikisha wataalam wa mazingira, kilimo na usimamizi wa kemikali na taka, kutoka katika Wizara na taasisi mbalimbali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Usimamizi wa Mkataba wa Stockholm hususan katika eneo la kujenga uwezo kwa wataalamu wa sekta, na taasisi zinazohusika na masuala ya kemikali zilizo chini ya Mkataba, ambao Tanzania ni mwanachama.