Shirika la ndege la Auric Air limeanzisha
safari mpya ya ndegeza kila siku kati ya Dar es Salaam na Morogoro
ikiwa ni mipango yake ya kuwafikia wananchi wengi katika mikoa mbalimbali
Tanzania.
Taarifa iliyotolewa
kupitia tovuti ya shirika hilo inaeleza kuwa safari hizo zitaanza
siku ya Ijumaa ya Novemba 15 mwaka huu ambapo nauli itakuwa ni dola 100 za kimarekani kwa
safari moja, nauli hiyo ikijumuisha gharama zote.
Ratiba ya safari zake itakuwa kama ifuatavyo:-
Ratiba ya safari zake itakuwa kama ifuatavyo:-
Itaondoka Dar es Salaam saa 11.15 jioni (17:15 hrs)
Itaondoka Morogoro saaa 12.30 asubuhi (06:30 am)