Facts: Mambo muhimu usiyoyajua kuhusu mnyama Twiga

Twiga ni mnyama mzuri ambaye Tanzania hutumia alama yake kama urithi wa Taifa.Twiga ni mnyama mrefu kuliko wote duniani.Ana miguu mirefu... thumbnail 1 summary
Twiga ni mnyama mzuri ambaye Tanzania hutumia alama yake kama urithi wa Taifa.Twiga ni mnyama mrefu kuliko wote duniani.Ana miguu mirefu,shingo ndefu sana,ulimi mrefu na pembe fupi zilizo butu.Mwili wake una mabaka yenye rangi ya kikahawia-njano na kuzungukwa na rangi ya maziwa.

Mnyama huyu anapatikana katika nyika hususan sehemu zenye migunga pamoja na mikakaya,miti ambayo huifurahia sana na ni chakula chake kikuu.Twiga hana ushindani mkubwa wa chakula na wanyama wengine kwa vile yeye hula majani ya juu nchani wakati wanyama wengine hawafikii majani hayo.

Twiga ana urefu wa kati ya mita 4.8 na 5.5 Uzito wake ni kati ya kilo 700 na 1500.Twiga jike ana rangi ng'avu zaidi kuliko dume.Hii inaweza kuwa ni maumbile ya kuwavutia Twiga dume.Dume ni mkubwa na mzito kuliko jike.

Urefu wa ulimi wake ni kati ya sentimeta 46 hadi 50 wakati ambapo urefu wa moyo ni meta 0.6 Ana uwezo wa kukimbia kilometeta 55 kwa saa.Mkia wake ambao ni meta 2.4 ni mrefu kuliko mikia ya wanyama wote duniani.

Twiga huzaa mtoto mmoja kwa mara moja na huweza kuishi kati ya miaka 20 hadi 30.Huchukua mimba kwa muda wa miezi 14.15 hadi 15.mtoto anapozaliwa huwa na uzito wa kati ya kilo 45 hadi 70 na urefu wa mita1.8

Shingo yake ndefu hufanya mwendo wake kuwa wa madaha na kuwavutia watu wengi.Akikimbia utampenda zaidi.

Utalii hususani wa wanyamapori na ndege ni moja ya vyanzo muhimu vya mapato ya nchi yetu.

TUSHIRIKIANE KUWALINDA WANYAMA NA KUYALINDA MAZINGIRA.
CHANZO: MALIASILI ZETU