Facts: Pamoja na mateke yake, Pundamilia ni mnyama mpole na mwenye huruma

Pundamilia ni nyama ambaye kwa lugha ya kitaalamu anajulikana kama 'equids' na kwa kiingereza anajulikana kama 'Zebra' .P... thumbnail 1 summary
Pundamilia ni nyama ambaye kwa lugha ya kitaalamu anajulikana kama 'equids' na kwa kiingereza anajulikana kama 'Zebra' .Pundamilia ni mnyama mkubwa mithili ya ng'ombe.Uzito wake ni taklibani kilogram 300 na uwezo wa kuishi ni miaka kama 20.Ana uwezo mkubwa wa kusikia,kuona na kukimbia kwa haraka kiasi cha kilometer 65 kwa saa.

Pindamilia ana miguu myembamba na mirefu kiasi,ambayo humuwezesha kutembea kwa urahisi na kukimbia.Ni mnyama jasiri asiyeogopa kupambana na adui zake kwa mateke.Adui wa pundamilia mara nyingi ni Simba,Fisi,Mbwa mwitu na Binadamu ambaye humwinda kwa ajili ya nyama na ngozi.

Mnyama huyu ana miraba mingi myeusi ya mkato usoni na miguuni.Pundamilia ana nywele ndefu kati ya masikio na ukwato mmoja kama wa Farasi na kihongwe ambao ni jamii yake.

Mistari ya Pundamilia humsaidia kujificha kutokana na maadui zake.Inaweze kuwa rahisi sana kumuona Pundamilia katika maeneo ya kawaida ya binadamu,lakini awapo porini hasa kukiwa na mwanga mwingi au giza si rahisi kwa adui kumuona kwa urahisi.

Mistari hiyo ambayo hutofautiona kutoka Pundamilia mmoja hadi mwingine huhuisha ulinzi dhidi ya maadui zake ambao adui huyo hawezi kumchukua Pundamilia mmoja katika kundi lake kwa urahisi.Kwa sababu huonekana kama wanafanana sana.

inasemekana chimbuko la pundamilia hasa ni kusini mwa Afrika na wao hupendelea zaidi kuishi kwenye maeneo ya mbuga na nyika.Pundamilia ni mnyama anaependa umoja na ushirikiano nawanyama wengine.Mara nyingi utamkuta na Swala,Twiga,Nyumbu n.k.

Pundamilia jike huchukua mimba akiwa na umri wa miaka mitatu na baada ya mwaka mmoja ndama wa pundamilia huwa amezaliwa.

Tabia ya kushangaza ya mnyama huyu,hupendelea kuishi katika familia yenye Pundamilia (5) watano hadi Ishirini(20) ambapo ,Pundamilia dume moja na majike kadhaa pamoja na Pundamilia wadogo huishi pamoja.Dume ndilo huwa na dhamana ya kuilinda familia hiyo na maadui.

Pundamilia ni mnyama mpole,mtulivu,mwenye huruma na ushirikiano.Mmoja wao akiugua na kushindwa kutembea kwa haraka ,kundi la familia hiyo hupunguza mwendo ili kuenenda pamoja na mwenzao ambaye ni mgonjwa.Aidha mmojawapo anapopotea familia hiyo huchukua jukumu la kumtafuta kwa siku kadhaa.

Hata hivyo,familia zenye pundamilia watano hadi 20 huungana na familia nyingine na kufanya kundi kubwa na kila kundi huwa na mpangilio wake.Pundamilia wazee hushabihiana kwa kiasi kikubwa lakini madume na majike mara nyingi hutengana na familia zao na kuunda familia nyingine.Aidha baadhi ya Pundamilia dume ambao hawana familia huungana na kuunda kundi la 'makapera'.

Pundamilia huwa makini sana wakati wa mchana,wakati wa usiku hupendelea kula sehemu zenye nyasi fupi ili kujikinga na maadui.Hutumia muda kama saa moja hivi kula na kutembeatembea.Wakiwa katika mapumziko baadhi ya Pundamilia hulala na mmoja hubakia kasimama akiwalinda wenzake na maadui ambao wanaweza kujitokeza.

TUSHIRIKIANE KUWALINDA WANYAMA NA KUYALINDA MAZINGIRA.
CHANZO: MALIASILI ZETU