Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa
Katavi imewahukumu watu watatu kutumikia kifungo cha jumla ya
miaka sabini jela bada ya kupatikana na hatia ya kukamatwa na
meno ya tembo manne yenye thamani ya shilingi milioni 45
Hukumu hiyo ilitolewa hapo jana na Hakimu Mkazi
mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa baada ya
kulidhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa
mashitaka na upande wa utetezi
Waliohukumiwa kifungo hicho ni Gwabi Mayala
(39) mkazi wa kijiji cha Majimoto Wilaya ya Mlele Mkoani
Katavi ambae alikuwa mshitakiwa wa kwanza amehukumiwa kifungo
cha miaka 30 na kulipa fidia ya shilingi milioni 45
Washitakiwa wengine waliohukumiwa ni Mashaka Mabanga
(33) Mkazi wa Sumbawanga Mkoa wa Rukwa na Adamu
Kalinzi (30) Mkazi wa Kijiji cha majimoto Wilaya ya Mlele Mkoani
Katavi wamehukumiwa kila mmoja kifungo cha miaka ishirini jela
Awali katika kesi hiyo ilidaiwa na mwanasheria wa
Serikali wa Mkoa wa Katavi Fadhili Mwandoloma kuwa washitakiwa
walitenda kosa hilo hapo Oktoba 10 mwaka huu majira ya
saa nne usiku katika Kijiji cha Majimoto Wilayani Mlele
Wanadaiwa siku hiyo ya tukio washitakiwa
walikamatwa wakiwa na meno manne ya Temboyenye uzito wa kilo kumi na
sita yenye thamani ya shilingi milioni 45 wakiwa katika harakati ya
kuyauz
Mwanasheria huyo wa Serikali aliiambia mahakama kuwa
Mshitakiwa wa kwanza Gwabi Mayala ndiye aliyekuwa
mwenye meno hayo ya Tembo na aliwashirikisha wenzake hao wawili
kwa ajiri ya kumtafutia wateja ambao wangeyanunua meno hayo ya
Tembo
Aliiambia mahakama baada ya washitakiwa hao kukamatwa
na Askari wa Hifadhi ya wanyama pori ya Katavi walioshirikiana na
polisi washitakiwa walipofikishwa polisi mshitakiwa wa pili na
watatu walikiri kuhusika na meno hayo ya tembo na kudai kuwa
meno hayo ni ya mshitakiwa wa kwanza Gwabi Mayala
Hakimu mkazi mfawidhi Chiganga baada ya
kusikiliza mwenendo mzima wa kesi hiyo aliiambi mahakama kuwa
kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo wa pande mbili za
mashitaka na utetezi mahakama imewaona washitakiwa wote watatu
wanahatia hivyo kabla ya mahakama haija towa adhabu inatowa nafasi
kwa washitakiwa kujitete
Katika utetezi washitakiwa Mashaka na Adamu
walikiri kukamatwa na meno hayo ya Tembo lakini walidaikuwa meno hayo
ya Tembo yalikuwa ni ya mshitakiwa wa kwanza Gwabi Mayala ambae
alikuwa amewaomba wamtafutie wateja wa kuyanunua kwa upande
wake mshitakiwa Gwabi aliiomba mahakama isikubaliane na maelezo ya
washitakiwa wenzake kuwa meno hayo yalikuwa sio ya kwake
Hakimu Chiganga alieleza mahakama kuwa
washitakiwa wamevunja sheria ya kifungu namba 86 (1) (2) cha sheria
ya huifadhi ya mwaka 2009 na kifungu namba 57 na 60 ya sheria
ya kuhujumu uchumi sura ya 200 ya mwaka 2002 hivyo mahakama
imetowa adhabu kwa mshitakiwa wa kwanza Gwabi Mayala kutumikia
kifungo cha miaka 30 jela la kulipa fidia ya shilingi milioni 45
ambayo ni thamani ya meno hayo ya Tembo
Pia washitakiwa Mashaka Mabanga na Adamu
Kalinzi wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja
baada ya kupatikana na hatia ya kushirikiana na mshitakiwa wa kwanza
katika biashara ya kumtafutia wateja wa kununua meno ya Tembo