Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa Tanzania
(Tanapa), Allan Kijazi, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo
pichani), katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam
jana. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa
Shirika
la Hifadhi za Taifa (Tanapa) limesema limejipanga nje na ndani ya nchi
ikiwamo kuwashirikisha wanakijiji wanaozizunguka hifadhi hizo kupambana
na ujangili.
Hatua hiyo imechukuliwa baada ya serikali kusitisha operesheni ya kutokomeza ujangili kutokana na kuwapo kwa madai ya vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya raia.
Hatua hiyo imechukuliwa baada ya serikali kusitisha operesheni ya kutokomeza ujangili kutokana na kuwapo kwa madai ya vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya raia.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa, Allan Kijazi, aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.
Alisema wameanzisha vikosi kazi kwa ajili ya kutoa elimu na misaada mbalimbali kwa wanakijiji ili kutatua matatizo yatakayojitokeza wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kutokomeza uhalifu.
“Tunatarajia kuwapatia mafunzo na vitendea kazi vya kisasa askari wa wanyamapori kwa kushirikisha polisi wa kimataifa (Interpol) ili kuimarisha mtandao wa kutokomeza ujangili nchini,” alisema.
Wakati zoezi la tokomeza ujangili linaendelea, Tanapa imetenga maeneo 34 ya uwekezaji kwa lengo la kuinua utalii Kusini na Magharibi mwa Tanzania kwa kupanua wigo wa huduma ya malazi.
Alisema maeneo yaliyotengwa yatakuwa kwa ajili ya ujenzi wa hoteli na kambi za kudumu kwa wageni zitakazopatikana katika Hifadhi ya Kilimanjaro, Katavi, Mikumi, Mkomazi, Ruaha, Saadani, Tarangire, Rubondo na Kitulo.
Kijazi alisema uamuzi wa kutenga maeneo hayo umezingatia ukuaji wa sekta ya utalii nchini. Asilimia 75 ya wageni wanaofika nchini hutembelea Hifadhi za Taifa.
Aidha, alisema shirika hilo limejipanga kuandaa miundombinu ya barabara, madaraja na viwanja vya ndege ili kurahisisha zoezi la uwekezaji kwenye maeneo yaliyoanishwa.
Alisema wameanzisha vikosi kazi kwa ajili ya kutoa elimu na misaada mbalimbali kwa wanakijiji ili kutatua matatizo yatakayojitokeza wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kutokomeza uhalifu.
“Tunatarajia kuwapatia mafunzo na vitendea kazi vya kisasa askari wa wanyamapori kwa kushirikisha polisi wa kimataifa (Interpol) ili kuimarisha mtandao wa kutokomeza ujangili nchini,” alisema.
Wakati zoezi la tokomeza ujangili linaendelea, Tanapa imetenga maeneo 34 ya uwekezaji kwa lengo la kuinua utalii Kusini na Magharibi mwa Tanzania kwa kupanua wigo wa huduma ya malazi.
Alisema maeneo yaliyotengwa yatakuwa kwa ajili ya ujenzi wa hoteli na kambi za kudumu kwa wageni zitakazopatikana katika Hifadhi ya Kilimanjaro, Katavi, Mikumi, Mkomazi, Ruaha, Saadani, Tarangire, Rubondo na Kitulo.
Kijazi alisema uamuzi wa kutenga maeneo hayo umezingatia ukuaji wa sekta ya utalii nchini. Asilimia 75 ya wageni wanaofika nchini hutembelea Hifadhi za Taifa.
Aidha, alisema shirika hilo limejipanga kuandaa miundombinu ya barabara, madaraja na viwanja vya ndege ili kurahisisha zoezi la uwekezaji kwenye maeneo yaliyoanishwa.
CHANZO:
NIPASHE