TANZANIA INAONGOZA KWA VIVUTIO VYENYE UBORA BARANI AFRIKA

Tanzania inaongoza kwa kuwa na vivutio bora vya utalii barani Afrika,utafiti uliondeshwa na mtandao wa safaribookings.com wa nchini uhola... thumbnail 1 summary
Photo: Tanzania inaongoza kwa kuwa na vivutio bora vya utalii barani Afrika,utafiti uliondeshwa na mtandao wa safaribookings.com wa nchini uholanzi umebainisha.Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) bw.Allan Kijazi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salam.Bw. Kijazi alibainisha kuwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ilikuwa ya kwanza kati ya vivutio 50 bora Barani Afrika ambapo vivutio 10 kati ya hivyo viko Tanzania.Alivitaja vivutio vilivyoongoza kuwa ni Ruaha,Mahale,Gombe,Katavi,Tarangire,ziwa Manyara na Arusha,Vingine ni Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na pori la akiba la selous.
Akizungumzia faida za kuwa na vivutio bora ,ndugu kijazi alisema kwamba wingi na ubora wa vivutio hivyo umetoa fursa ya pekee kwa wawekezaji kuwekeza kwenye maeneo mbalimbali katika hifadhi hizo hivyo kuongeza pato la Taifa.

Aidha ndugu Kijazi aliongeza kwamba TANAPA imetenga maeneo 34 kwa ajili ya kupanua wigo wa huduma za malazi katika hifadhi  za Taifa ambapo kipaumbele ni kwenye hifadhi za kusini na magharibi ya nchi ambazo zina uhaba wa malazi na hivyo kusababisha idadi ndogo ya watalii kutembelea maeneo hayo.
Bw. Kijazi alimaliazia kwa kusema kwamba wanategemea kuongeza idadi ya watalii kutokana na maboresho hayo na hivyo kukuza pato la Taifa kutokana na sekta ya utalii.

KWA HISANI YA MATUKIO NA MICHAPO BLOGTanzania inaongoza kwa kuwa na vivutio bora vya utalii barani Afrika,utafiti uliondeshwa na mtandao wa safaribookings.com wa nchini uholanzi umebainisha.Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) bw.Allan Kijazi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salam.Bw. Kijazi alibainisha kuwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ilikuwa ya kwanza kati ya vivutio 50 bora Barani Afrika ambapo vivutio 10 kati ya hivyo viko Tanzania.Alivitaja vivutio vilivyoongoza kuwa ni Ruaha,Mahale,Gombe,Katavi,Tarangire,ziwa Manyara na Arusha,Vingine ni Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na pori la akiba la selous.
Akizungumzia faida za kuwa na vivutio bora ,ndugu kijazi alisema kwamba wingi na ubora wa vivutio hivyo umetoa fursa ya pekee kwa wawekezaji kuwekeza kwenye maeneo mbalimbali katika hifadhi hizo hivyo kuongeza pato la Taifa.

Aidha ndugu Kijazi aliongeza kwamba TANAPA imetenga maeneo 34 kwa ajili ya kupanua wigo wa huduma za malazi katika hifadhi za Taifa ambapo kipaumbele ni kwenye hifadhi za kusini na magharibi ya nchi ambazo zina uhaba wa malazi na hivyo kusababisha idadi ndogo ya watalii kutembelea maeneo hayo.
Bw. Kijazi alimaliazia kwa kusema kwamba wanategemea kuongeza idadi ya watalii kutokana na maboresho hayo na hivyo kukuza pato la Taifa kutokana na sekta ya utalii.