HATIMAYE WAJERUMANI WAREJESHA JINO LA MTWA MKWAWA

Chifu Abdul Adam Sapi Mkwawa akionyesha jino la Mtwa Mkwawa lililorejeshwa na Wajerumani hivi karibuni katika  kilele cha Maadhimis... thumbnail 1 summary
jino_aa6c0.jpg

jino2_4a809.jpg
Chifu Abdul Adam Sapi Mkwawa akionyesha jino la Mtwa Mkwawa lililorejeshwa na Wajerumani hivi karibuni katika  kilele cha Maadhimisho ya Chifu Mkwawa na Utamaduni wa Mkoa wa Iringa yaliofanyika katika Kijiji cha Kalenga leo wilayani Iringa. Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Naibu Waziri wa Maji Dkt. Bilinithi Mahenge (kushoto) kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda. (Picha na Friday Simbaya)
JESHI_ae06a.jpg
HISTORIA FUPI
Kwa  mujibu wa historia, Mtwa Mkwawa, alizaliwa mwaka 1855 katika Kijiji cha Luhota wilayani Iringa. Mkwawa aliongoza jeshi katika vita vya kupinga kutawaliwa na wakoloni wa kijerumani. Mkwawa alifanikiwa kuwafukuza na kuwaua wajerumani 1000 mwaka 1891 katika eneo la Lugalo wilayani Kilolo.
Tarehe 30.10.1894, Ujerumani ulifanikiwa kuvamia na kuiteka ngome ya Mkwawa katika Kijiji cha Kalenga. Mkwawa alifanikwa kuwatoroka askari wa kijerumani na kuendeleza vita vya msituni kwa miaka minne zaidi hadi alipozidiwa nguvu na kuamua kujiua mwenyewe kwa risasi tarehe 19 Julai,1898 katika eneo la Mlambalasi ambako kumejengwa mnara wa kumbukumbu uliozindiliwa rasmi na muasisi na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1998. (FRIDAY SIMBAYA)