Wawekezaji
wote Nchini wanatakiwa kuhakikisha wanaacha kutumia magogo katika
uzalishaji badala yake watumie tekinolojia ya kisasa ili kuepuka
mabadiliko ya tabia ya nchi na uchafuzi wa Mazingira yanayotokana na
ukataji miti.
Hayo
yamesemwa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Mh.Dkt. Injinia Binilith Mahenge wakati alipofanya ziara ya
kutembelea kiwanda cha kutengeneza sabuni na mafuta ya kupikia (BIDCO)
kilichopo mikocheni jijini Dar es Salaam.
Amekiagiza
kiwanda hicho kuacha mara moja matumizi ya magogo kwani inaathari kubwa
sana kwa jamii. Hata hivyo amesema kuwa atatembelea tena kuangalia
kama wameacha kutumia magogo ndani ya miezi sita, endapo watabainika
wanaendelea kutumia magogo,hatua kali itachukuliwa juu ya Kiwanda hicho
endapo watakiuka masharti waliyopewa.Amesema Kiwanda kitafungwa mara
moja.
Hata
hivyo Mh. Mahenge amewaomba wawekezaji wa viwanda vingine kuiga mfano
wa kiwanda cha Coca Cola katika utunzaji wa Mazingira, kwani wao ni
mfano mzuri kwa viwanda vingine kwa kuanzisha technolojia nyengine ya
kuchunguza maji taka kama ni salama kwa viumbe hai.
Amemalizia
kwa kusema "Tunapenda wawekezaji lakini ni wale wanaotunza na kuyaenzi
mazingira kwa usalama wa wananchi na nchi yetu kwa ujumla".
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith
Satano Mahenge ( wa pili kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Mazingira
Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Julius Ningu (wa kwanza kushoto), wakiwa
katika ziara fupi ya ukaguzi wa mazingira katika kiwanda cha Coca Cola
kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. Wakiwa pamoja na mkurugenzi wa
uzalishaji soda katika kiwanda hicho Bw. Louis Coetzee (wa kwanza
kulia).
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira Dkt. Injinia Binilith
Satano Mahenge (wa pili kulia), akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa
uzalishaji soda Bw. Louis Coetzee ( wa kwanza kulia), akielezea jinsi
kiwanda hicho kinavyotumia maji taka kulinda Mazingira ya kiwanda.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Dkt. Injinia Binilith
Mahenge, akiongea na Vyombo vya habari kuhusu ziara yake na kuwaambia
kwamba nchi inahitaji wawekezaji wanaotunza na kulinda Mazingira yetu.
Viwanda alivyovitembelea ni kiwanda cha kuzalisha Mafuta ya kula na
sabuni (BIDCO), M.M.I steel mill kinachozalisha Nondo na Mabati pamoja
na kiwanda cha Coca Cola vilivyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.