Wizara yaanzisha programu ‘Panda Miti Kibiashara’

WIZARA ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland, imeanzisha programu ya Panda Miti Kibishara (Privat... thumbnail 1 summary
WIZARA ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Finland, imeanzisha programu ya Panda Miti Kibishara (Private Forestry Programme).
Mradi huo una lengo la kuwahamasisha wananchi kupanda miti kwa kuzingatia kuwa ni zao la biashara.

Taarifa iliyotumwa na Meneja Uenezi wa Programu hiyo, George Matiko, inaeleza ingawa programu hiyo imeshiriki kwa mara ya kwanza katika maonyesho ya Sabasaba ilikuwa kati ya sehemu zilizowavutia watu wengi.

“Wananchi waliotembelea waliuliza maswali kuhususiana na aina za miti ya mbao inayofaa kupandwa katika sehemu zao na upatikanaji wake,” alisema.

Alieleza programu ya ‘Panda Miti Kibiashara; inatekelezwa katika wilaya za Ludewa, Makete, Njombe, Kilolo, Mufindi na Kilombero.

Alisema lengo la programu hiyo ni  kuongeza kipato cha wananchi  waishio  vijijini kwa kupanda miti.
Katika programu hiyo imeazimiwa kuwa jumla ya hekta 15,000 zitapandwa miti na wananchi waliojiunga na vikundi vya wakulima wa miti.