Shirika la kutetea haki za wanyama la Afrika Kusini limeanza uchunguzi
kuhusiana na kifo cha twiga baada ya kuumia wakati akisafirishwa kwenye
gari. Watu walioshuhudia tukio hilo wanasema twiga mmoja kati ya wawili
waliokuwa kwenye lori, aligonga kichwa chake katika barabara moja mjini
Johannesburg. Gari hilo baadaye liliharibika na kulazimika kusubiri kwa
saa kadhaa kabla ya kutengenezwa. Wanyama wote wawili walipelekwa kwa
daktari wa wanyama, lakini shirika la kutetea haki za wanyama la NSPCA
limesema twiga mmoja alikufa. Tukio hilo limeleta mjadala mkubwa kwenye
mtandao wa kijamii wa Twitter. Meneja wa NSCPA Rick Allen amethibitisha
kuwa twiga huyo alipata majeraha ya kichwani lakini amesema uchunguzi ni
muhimu ufanyike kutafuta sababu hasa ya kifo hicho.