Mapigano makali: Mwanamke amuua Chui baada ya kupigana nae kwa muda wa nusu saa

 Madaktari wakimpatia matibabu mwanamke aliyeua Chui Mama mwenye umri wa miaka 54, Kamla Devi amefanikiwa kumuua Chui baada ya ku... thumbnail 1 summary


 Madaktari wakimpatia matibabu mwanamke aliyeua Chui

Mama mwenye umri wa miaka 54, Kamla Devi amefanikiwa kumuua Chui baada ya kupigana nae kwa takribani dakika 30 huko India.

Mkasa huo ulimkuta mwanamke huyo akiwa katika harakati za kurudi nyumba baada ya kuhitimisha shughuli za shamba ndipo njiani mama akakutana na Chui ndipo vurugu zikaanza, kwakuwa mama huyo alikuwa na mundu na jembe dogo aliweza kumdhibiti mnyama huyo asiweze kumzuru.

Mapigano hayo yalidumu kwa dakika kadhaa baada ya kila mmoja kujeruliwa, ila mama huyo alipoteza nguvu nyingi kutokana na kuvuja damu sana kabla ya kupata msaada, na baadae watu walimtafuta Chui na kumkuta.

Mama huyo anaendelea na matibabu katika hospital kuu ya India.

 Kuna wanaume wanajifanya wababe sana na kuwaonea wanawake kwa kuwapiga au kuwanyanyasa, sasa wamfuate na huyo mama wakakione cha moto, Chui kafa! Wewe sijui atakufanyaje huyu mama, tusiwachukulie poa wanawake wako fiti pia.