Kama
ni kweli basi nchi hii inahitaji maombi. Ikiwa bado Tanzania
inakabiliwa na skendo ya pembe za ndovu zinazodaiwa kuondoka na ndege ya
rais wa China alizuru nchini, kashfa nyingine kubwa imezuka!
Tanzania
inashutumiwa kurejesha mpango wa kuwahamisha wamasai 40,000 katika eneo
waliloishi kwa miaka na miaka, ili kuipa eneo hilo familia ya kifalme
ya Dubai kwaajili ya kuwinda wanyama.
Mwaka
jana serikali ilidai kuahirisha mpango wa kutenga eneo la kilomita ya
mraba 1,500 zinazotengenisha mbuga ya wanyama ya Serengeti kwa matumizi
uwindaji wa biashara utakaofanywa na kampuni yenye makazi yake kwenye
falme za kiarabu, Ortelo Business Corporation (OBC).
Na sasa gazeti la The Guardian
na Uingereza na mengine, yameandika kuwa mpango huo umerejea na wamasai
hao wameamrishwa kulihama eneo hilo kufikia mwishoni mwa mwaka huu.
Wawakilishi
wa wananchi hao wanakutana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, bungeni
Dodoma kuelezea hasira yao. Wanadai kuwa kuondolewa kwenye ardhi hiyo ni
kunyang’anywa kwa urithi wao na maisha ya watu 80,000 yataathirika.
Eneo hilo ni muhimu kwa malisho ya mifugo ya wananchi hao wanaoishi kwa
kutegemea ufugaji.
Serikali itawalipa shilingi bilioni moja kama fidia ambazo wamasai wamezikataa.
“Nahisi kusalitiwa,” mratibu wa kikundi cha Ngonett Samwel Nangiria ameliambia The Guardian.
“Bilioni moja ni ndogo saba huwezi kulinganisha na ardhi. Imerithiwa. Mama na bibi zao wamezikwa kwenye ardhi ile. Hakuna cha kulinganisha nayo.”
“Bilioni moja ni ndogo saba huwezi kulinganisha na ardhi. Imerithiwa. Mama na bibi zao wamezikwa kwenye ardhi ile. Hakuna cha kulinganisha nayo.”
Msemaji
wa wizara ya Maliasili na Utalii, ameliambia gazeti hilo kuwa hana
taarifa kuhusiana na mpango huo. Habari hiyo imeandikwa Jumatatu kwenye
magazeti na vyombo vingi vikubwa vya habari duniani likiwemo Daily Mail, rt.com ya Urusi, eTurboNews, The Week Uk, Europa Press, Ecoblog.it na vingine.
Chanzo: Bongo5