Na Freddy Macha, London
Watalii
na wageni Tanzania wamehakikishiwa kwamba kasheshe ya Ebola
inayousakama uwanda wa magharibi ya bara haitaidhuru Bongo.
Akizungumza nami katika ofisi ya kampuni ya Safari Hub yenye makao makuu
Arusha na London, Mkurugenzi, Navraj Hans alisema ingawa kitakwimu
idadi ya watalii barani imeshuka kwa asilimia 50 hakuna haja ya kuhaha.
“Ebola inasambaa kirahisi zaidi kuelekea Ulaya kutoka Afrika Magharibi kuliko kuja kwetu. Sisi tuko mbali sana.”
Bwana
Hans ambaye pia ni dereva na mshindi wa mbio za magari Tanzania,
alisema ni muhimu kuzingatia si Ebola tu nuksi iliyolipaka bara, masizi.
“Hebu tazama Afrika Kusini yenye mauaji makubwa sana, kitakwimu,
duniani. Utalii unaendelea kama kawaida, maana wenzetu wanasisitiza kuwa
kuna mabaya machachena mazuri mengi zaidi. Matokeo,” aliendelea
kufafanua Bwana Hans ambaye ni mzawa wa Arusha,
“Watalii wanaendelea kutiririka Sauzi bila shaka yeyote.”
Mkurugenzi huyu wa Safari Hub aliendelea kusisitiza kuwa Tanzania ni moja ya nchi zinazoongoza kwa mandhari nzuri duniani.
“Watanzania
wanasifika kwa ukarimu wao na amani. Hivyo tujitangaze zaidi. Tujifunze
toka kwa nchi kama Singapore na Indonesia wanaojua kujitangaza.”
Kuonyesha namna Tanzania inavyohusudika, Bwana
Hans alisema karibuni kampuni ya kimataifa ya Kili Villa imeamua
kujenga uwanja wa mchezo wa Golf eneo la Maji ya Chai wilaya ya Arumeru.
Ili kutimiza lengo lake, kampuni hiyo iliwasiliana na Safari Hub.
Uwanja huo utakaokuwa na ekari 7,000 na mashimo 18, umeshawekwa katika
ya orodha ya viwanja kumi bora vya golf Afrika.
Mandhari
ya uwanja inaonyesha milima Meru na Kilimanjaro, moja ya vivutio vikuu
vya Kitanzania.
Bosi wa Kili Villa, Bwana Wilhem Kurpers alinieleza kwamba mcheza Golf
mashuhuri, Tiger Woods, ameshakubali mualiko kuitembelea Tanzania kwa
kuvutiwa na viwanja hivyo vya Maji ya Chai.
Mapema
mwaka huu Safari Hub ikishirikiana na shule maarufu ya Eton College na
Ubalozi wetu Uingereza ilipeleka timu ya vijana kuendeleza mpira Arusha.
Mandhari ya uwanja mpya wa gofu utaojengwa eneo la Majani ya Chai Arusha na kampuni ya Kili Villa
Mandhari ya uwanja mpya wa gofu utaojengwa eneo la Majani ya Chai Arusha na kampuni ya Kili Villa
Mkurugenz wa Safari Hub Bw. Navraj Hans akiwa ofisini kwake na Bosi wa kampuni ya Kili Villa Bw. Wilhem Kurpers
Bw. Navraj Hans akiwa na Bosi wa kampuni ya Kili Villa Bw. Wilhem Kurpers mbele ya picha za vivutio vya Tanzania
Mkurugenzi
wa Safari Hup Dilip Navapurkar akizungumza, akisema Tanzania inaweza
kuendelezwa ikafikia kiwango cha timu nyingine bora Afrika katika
kandanda.