Matangazo
ya barabarani (billboards) yenye picha za wanawake waliovaa nguo za
mitego huwachanganya madereva na yanaweza kusababisha ajali, utafiti
umesema.
Watafiti kwenye chuo kikuu cha Alberta wamebaini kuwa matangazo yenye picha za aina hizo huathiri tabia za uendeshaji.
Utafiti
huo ulionesha kuwa matangazo ya aina hiyo yana madhara ikiwemo
kuhatarisha usalama wa watu, kuongezeka kwa kugongana magari na
kusababisha foleni za magari kwenda taratibu.
Imehaririwa na Bongo5
Chanzo: Sunday World