PACJA yatoa mafunzo kwa waandishi wa habari Afrika ili kuwajengea uwezo wa kuripoti habari za mazingira kuelekea COP21, Paris Ufaransa

Mtandao wa haki za mazingira Barani Afrika (Pan African Climate Justice Allience PACJA), kwa kushirikiana na Mtandao wa wandishi wa habari ... thumbnail 1 summary
Mtandao wa haki za mazingira Barani Afrika (Pan African Climate Justice Allience PACJA), kwa kushirikiana na Mtandao wa wandishi wa habari za mabadiliko ya tabianchi Zambia (ZCCN) wameandesha warsha ya siku mbili kwa waandishi wa habari za mazingira barani Afrika.

Warsha hiyo inayofanyika mjini Lusaka, Zambia imewashirikisha waandishi wa habari wapatao 30 kutoka nchi mbalimbali za Afrika kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kuripoti habari za mabadiliko ya tabianchi kuelekea kwenye mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi    (COP21) utakaofanyika mjini Paris, Ufaransa Desemba 2015.

Waandishi wa habari za mazingira walioshiriki warsha hiyo kutoka Tanzania ni Dotto Kahindi na Suleiman Shaban 
Waandishi wa habari za mazingira kutoka nchi mbalimbali za Afrika wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa ufunguzi wa warsha ya mabadiliko ya tabianchi unaolenga kuwanoa waandishi hao kuweza kuripoti habari za mkutano wa mazingira wa kimataifa COP21 utakaofanyika mjini Paris Ufaransa.
 Mwakilishi wa UNFCCC nchini Zambia, Richard Lungu akizungumza na waandishi wa habari
Mkufunzi wa warsha hiyo, Wanjoh Kabukuru kutoka Kenya akifafanua umuhimu wa waandishi wa habari kuwa wabunifu katika kuandika habari za mabadiliko ya tabianchi ili ziweze kueleweka kwa jamii
 Webstar Whade kutoka Mtandao wa Mabadiliko ya tabianchi na maarifa Afrika (CDKN) akiwa na mwanachama wa PACJA Zambia, Robert Chimambo 

Mwandishi wa habari za sayansi na mzingira Sophie Mbugua (kushoto) kutoka Kenya akiwa na Mhariri wa jarida la mtandaoni la mazingira la Nigeria (EnvironewsNigeria) Michael Simire wakati wa warsha hiyo
Waandishi wa habari za mazingira kutoka Madagascar Rivonala na mwandishi Twahinwa Aimabue kutoka Rwanda 

#PanAfricanRoadtoParis