Tuwaeleze watoto wetu ukweli wa athari za mabadiliko ya tabianchi-Waziri Sitta

Watanzana wametakiwa kutunza na kuthamini mazingira kwa sababu ni urithi wa thamani kubwa sana kwa kizazi cha sasa na kijacho.  Hay... thumbnail 1 summary
Watanzana wametakiwa kutunza na kuthamini mazingira kwa sababu ni urithi wa thamani kubwa sana kwa kizazi cha sasa na kijacho. 

Hayo yamesemwa na Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya siku ya  mazingira Duniani, Mheshimiwa Samuel Sita- Waziri wa Uchukuzi ambaye alimuwakilisha Makamu wa Rais Mhe. Mohammed  Gharib Bilal.

Akiongea na Wananchi katika viwanja vya Tangamano vilivyopo katika jiji la Tanga Mheshimiwa Sita amesisitiza juhudi zaidi katika suala zima la utunzaji wa mazingira na kuwaomba Wazazi kuelemisha watoto wao umuhimu wa kuthamini mazingira. 

Aidha amewapa hongera Wananchi na Viongozi wa jiji la Tanga kwa kutilia mkazo usafi wa mazingira na kufanya jiji hilo kuibuka mshindi wa tatu katika mashindano ya usafi wa mazingira kitaifa.

Akimkaribisha Mgeni Rasmi ili kufungua sherehe hizo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Binilith Mahenge aliesma ni jukumu la kila mmoja kutunza na  kuhifadhi mazingira hivyo basi kila Mwananchi ajitahidi  katika hilo. 

Siku ya mazingira duniani hufanyika kila tarehe tano ya mwezi Juni kila mwaka. Kauli mbiu ya mwaka huu ni Ndoto bilioni saba, dunia Moja ,  tumia Rasilimali kwa uangalifu. Hii ikimaanisha kutumia vema rasilimali zetu ili kutunza vema mazingira yetu.