Mahakama kuu ya Kenya imemuachilia kwa dhamana mshukiwa mkuu wa uwindaji haramu aliyekamatwa nchini Tanzania.
Feisal
Mohammed Ali,aliyeorodheshwa katika nafasi ya sita ya watuhumiwa wa
uwindaji haramu na biashara ya kuuza pembe za ndovu ameachiliwa kwa
dhamana baada ya mawakili wake kuomba mahakama hiyo imruhusu apokee
matibabu .
Hata hivyo afisi ya kiongozi wa mashtaka ya umma nchini
humo tayari imeonesha kutoridhishwa kwake na uamuzi uliofikiwa na
hakimu Davis Karani katika mahakama ya Mombasa.
Hii si mara ya kwanza kwa mahakama za Kenya kumruhusu mshukiwa huyo kuondoka.
Mwezi
Machi,Feisal alipewa dhamana na mahakama ya Mombasa lakini afisi ya
kiongozi wa mashtaka ya umma ikakata rufaa iliyokubaliwa na mahakama ya
juu.
Hapo jana hakimu Karani alimpa Feisal dhamana ya shilingi millioni kumi za Kenya sawa na dola laki moja $100,000 za mMarekani
Feisal
anakabiliwa na shtaka la usafirishaji kinyume cha sheria kwa tani
mbili za pembe za ndovu yenye thamani ya dola milioni $4.5 za Marekani,
umiliki wa pembe za ndovu kinyume cha sheria.
Yamkini Feisal anatuhumiwa kuwa mmiliki wa pembe za ndovu 114.
Upande
wa mashtaka unadai kuwa yeye ndiye kiunganishi kati ya wawindaji haramu
wanaolaumiwa kwa kuuwa tembo 33,000 kati ya mwaka wa 2010-2012 barani
Afrika.
Feisal amekanusha mashtaka yote dhidi yake.
Kasha la pembe hizo za ndovu zilikuwa zimefichwa katika bohari moja ya wauzaji magari mjini Mombasa.
Punde
baada ya polisi kuvamia eneo hilo Feisal alitorokea Tanzania
alikokamatwa na polisi wa huko baada ya ombi kutolewa kupitia mtandao wa
polisi wa kimataifa Interpol.