ForumCC yazindua ripoti ya fedha za mabadiliko ya tabianchi kwenye sekta za Kilimo na Mifugo

ForumCC imezindua ripoti yake ya fedha za mabadiliko ya tabianchi kwenye sekta za kilimo na mifugo baada ya kufanya utafiti kwenye wilay... thumbnail 1 summary
ForumCC imezindua ripoti yake ya fedha za mabadiliko ya tabianchi kwenye sekta za kilimo na mifugo baada ya kufanya utafiti kwenye wilaya za Kilosa, Njombe, Singida na Kongwa.

Akiielezea ripoti hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya ForumCC, Euster Kibona anasema hakuna pesa zilizotengwa kutoka kwenye bajeti ya serikali katika sekta hizi zinazolenga kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

“Umefika wakati sasa kwa kuangalia uwezekano wa utafutaji wa fedha katika kulinda na kuhifadhi mabadiliko ya tabianchi ili kupunguza madhara yanayotokana na mabadiliko hayo ya hali ya hewa” anasema Kibona 

Ripoti hiyo imeonyesha pia kuwa pamoja na fedha za mabadiliko ya tabianchi kutolewa kwa kiasi kidogo sana lakini bado zimekosa usimamizi mzuri, uwazi wa matumizi yake na ukosefu wa uwakilishi stahiki kwa wadau na washirika katika eneo husika.
Mkuu katika kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Shakwaande Natai (kulia) akizindua ripoti hiyo ya fedha za mabadiliko ya tabianchi kwa kuipakia (upload) kwenye tovuti ya forumcc, huku akipata maelekezo ya namna ya kufanya hivyo kutoka kwa Afisa Miradi ForumCC, Fazal Issa.
Mkuu katika kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Shakwaande Natai akiwa na baadhi ya viongozi wa Bodi ya ForumCC, Wizara ya Kilimo na wadau wengine wa mabadiliko ya tabianchi.
 Wadau wa mabadiliko ya tabianchi wakifuatilia uzinduzi wa ripoti hiyo