KAMPENI YA UHAMASISHAJI JUU YA MABADILIKO YA TABIANCHI KUPITIA UENDESHAJI WA BAISKELI YAANZA MBEYA

Waendesha baiskeli kutoka Malawi wakiwasili kwenye mpaka wa Tanzania na nchi hiyo tayari kwa kukabidhi kijiti cha kampeni hiyo kwa wenza... thumbnail 1 summary
Waendesha baiskeli kutoka Malawi wakiwasili kwenye mpaka wa Tanzania na nchi hiyo tayari kwa kukabidhi kijiti cha kampeni hiyo kwa wenzao wa Tanzania.
Mmoja wa waendesha baiskeli Tanzania ambaye pia ni Ofisa Miradi wa Norwegian Church Aid, Tanzania, Gilbert Mworia.
Meneja Miradi wa shirika la Norwegian Church Aid, Augustina Mosha akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji juu ya mabadiliko ya tabianchi kupitia uendeshaji wa baiskeli.
Waendesha baiskeli wa Tanzania wakiwa katika mji wa Kyela Mbeya
Mama Mosha akiwa na baadhi ya waendesha baiskeli wa Tanzania
Balozi wa kampeni ya We Have Faith nchini Malawi, Father George Buleya (kushoto) akiwa na Mratibu wa Vijana kutoka YouthCAN Tanzania, Francisca Damian wakati wa hafla ya kukabidhiana kampeni hiyo iliyofanyika kwenye mji wa Kasumulu, Mbeya.

Na Dotto Kahindi

Kampeni ya uhamasishaji juu ya mabadiliko ya tabianchi kupitia uendeshaji wa baiskeli katika nchi mbalimbali Barani Afrika imeingia Tanzania Octoba 17 kwa waendesha baiskeli 21 kutoka Tanzania kuwapokea wenzao kutoka Malawi.

Kampeni hiyo ambayo imeanzia Msumbiji, Afrika Kusini, Botswana, Zimbabwe, Zambia, Malawi na hatimaye Tanzania na itatia nanga Kenya mapema mwezi novemba mwaka huu.

Msafara huo wa waendesha baiskeli kwa Tanzania umeanzia kwenye mpaka wa Tanzania na Malawi wa Kasumulu ambapo unataratia kwenda mpaka Namanga watakapoukabidhi kwa waendesha baiskeli wa Kenya.

Kwa mujibu wa Meneja Miradi wa shirika la Norwegian Church Aid, Augustina Mosha lengo la msafara huo ni kujenga uelewa kwa jamii juu ya mabadiliko ya tabianchi kwa kutumia vijana kutoka kwenye taasisi za kidini nchini.

Anasema msafara huo utahusisha pia uchukuaji wa saini za wananchi ili kuweka imani zao kwa viongozi wa kiserikali ambao watakwenda kwenye mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP21 utakaofanyika Desemba mwaka huu huko Paris, Ufaransa.

Mama Mosha anasema kuwa wameamua kutumia uendeshaji wa baiskeli kama njia ya kuhamasisha jamii juu ya mabadiliko ya tabianchi kwa sababu chombo hicho ni rafiki wa mazingira na hakichangii uzalishaji wa hewa ukaa.

Picha zote na tabianchi blog