Wadau wakutana Dar kujadili Mkataba Mpya wa Mabadiliko ya Tabianchi ‘Paris Agreement’

Ikiwa ni siku chache baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Nchi Wanachama COP21 uliokuwa ukifanyika Paris, Ufar... thumbnail 1 summary
Ikiwa ni siku chache baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Nchi Wanachama COP21 uliokuwa ukifanyika Paris, Ufaransa, ambao ulimalizika kwa kupitisha mkataba mpya wa mabadiliko ya tabianchi (Paris Agreement), wadau mbalimbali wamekutana kujadili matokeo ya mkutano huo.

Mkutano huo wa wadau umeandaliwa na ForumCC kwa kushirikiana na Rosa Luxemburg Stiftung (RLS) kwa lengo la kuangalia mazidi na mapungufu ya mkataba huo ambao umeweka historia mpya ya kuelekea juhudi za kupunguza ongezeko la joto duniani, kukabiliana na kupunguza madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Miongoni mwa vipengele vya mkataba huo vilivyojadiliwa na wadau hao ni pamoja na Kiwango cha nyuzi joto, Upunguzaji wa gesi Joto, Kukabiliana na mabadiliko ya tabainchi, Uharibifu na upotevu, Fedha za mabadiliko ya tabianchi, Mfumo wa taasisi na ushiriki wa serikali, waandishi wa habari pamoja na asasi za kiraia kwenye kuleta mchango wa makubaliano ya mkataba huo.

 Picha ya pamoja ya Wadau hao
Mwakilishi wa ForumCC, Adam Athony akitoa mrejesho wa kilichojiri kwenye Mkutano wa Mbadailiko ya Tabianchi COP21 uliofanyika Paris, Ufaransa
Mwakilishi wa Rosa Luxemburg Stiftung (RLS) Afrika Mashariki, Musa Bulegeya (katikati) akizungumza jambo wakati wa mkutano huo, kulia kwake ni Meneja Miradi ForumCC Rebecca Muna, wakati kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya ForumCC Yunista Kibona.
Mwandishi wa habari na Mmiliki wa mtandao wa Tabianchi, Dotto Kahindi akitoa mrejesho wa yale aliyojifunza kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabianchi COP21, Uliofanyika Paris, Ufaransa.
 Washiriki wakifuatilia mkutano huo
Mwakilishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Ladslaus Kyaruzi akielezea namna Tanzania ilivyoshiriki kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabianchi COP21. Picha zote na Jonathan Sawaya wa ForumCC