Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi
(kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha
(katikati) na Mkurugenzi wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini
mwa Jangwa la Sahara, Antois van der Westhuizen (kulia) wakipiga picha
ya kumbukumbu mara baada ya kusaini hati ya makubaliano na Benki ya NMB
itakayo wawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zaoKutoka
kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert
Mponzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha na
Mkurugenzi wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la
Sahara, Antois van der Westhuizen wakiwa katika tukio hilo lilifanyika
jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.Sehemu
ya waandishi wa habari wakishuhudia hafla ya kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.Sehemu
ya wanufaika wa mkopo huo wakishuhudia hafla ya kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi
Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha akizungumza katika tukio
la kutiliana saini ya makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya
John Deere (wauzaji wa matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa
matrekta kwa ajili ya shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye
Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi
akizungumza katika tukio la kutiliana saini ya makubaliano kati ya Benki
ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa matrekta) kuwawezesha
wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya shughuli zao. Tukio hilo
lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi
wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara,
Antois van der Westhuizen akizungumza katika tukio la kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.[caption id="attachment_66172" align="alignnone" width="800"]Sehemu
ya waandishi wa habari wakishuhudia hafla ya kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kushoto)
akisaini hati ya makubaliano na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) itakayo wawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa
ajili ya shughuli zao. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya John
Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Antois van der
Westhuizen na Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha wakishuhudia.Mkurugenzi
wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara,
Antois van der Westhuizen (kulia) akisaini hati ya makubaliano na Benki
ya NMB itakayo wawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa
Benki ya NMB, Filbert Mponzi na Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania
Ltd, Lukas Botha, tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden
Tulip jijini Dar es Salaam.
BENKI
ya NMB kwa kushirikiana na Kampuni maarufu kwa uuzaji wa matrekta ya
John Deere zimeingia makubaliano ili kufanikisha kuwakopesha matrekta
wakulia wanaochipuki kwa lengo la kuwawezesha waendelee kufanya vizuri
kwenye kilimo cha kisasa. Katika makubaliano hayo yaliyofanyika jijini
Dar es Salaam Banki ya NMB imekubali kutoa mkopo ambao utamuwezesha
mkulima kununua trekta hilo huku akiurejesha taratibu, Hata hivyo
Kampuni ya John Deere itatoa mafunzo ya kilimo cha biashara kwa mkulima
aliyenufaika na mkopo huo pamoja na kumfundisha matumizi bora ya kifaa
hicho cha kilimo.
Akizungumza
mara baada ya kutiliana saini ya makubaliano hayo, Mkuu wa Kitengo cha
Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi alisema benki yao
inatambua umuhimu wa sekta ya kilimo na inavyochangia kukuza uchumi wa
Tanzania hivyo kuamua kuwawezesha wakulima ili kuchochea ukuaji wa
uchumi kwa ujumla. "...Upatikanaji wa mikopo kwa wakulima siku za nyuma
ulikuwa ni kikwazo kikubwa katika maendeleo ya kilimo...hivyo
makubaliano haya yanakuja kuleta suluhisho kwa wakulima hasa katika eneo
la kupata vifaa muhimu vya kilimo cha kisasa kama matrekta yanayoendana
na mabadiliko ya teknolojia," alisema Mponzi.
Alisema
kwa kutambua mchango wa sekta ya kilimo tayari Benki ya NMB imewasaidia
wakulima wadogo zaini ya 600,000 kupata mitaji ya mikopo kwa ajili ya
uzalishaji wa mazao anuai ya kilimo pamoja na kuendesha mafunzo ya
kijasiliamali kuwajengea uwezo makundi yote. Kwa upande wake Mkurugenzi
wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara,
Antois van der Westhuizen alisema mikopo hiyo inayotolewa kwa wakulima
inalengo la kuwainua wakulima wadogo ili waweze kubadili kilimo chao
kuwa kilimo endelevu kinachotumia vifaa vya kisasa yakiwemo matrekta ya
kilimo, kuvunia na kusafirisha mazao kutoka shambani hadi eneo
linalokusudiwa.
"Kwa
kutambua umuhimu wa wakulima wadogo katika nchi za Afrika, John Deere
kwa kushirikiana na NMB tunategemea kuweka mifumo itakayowawezesha
wakulima wadogo ili kuleta ufanisi katika shughuli nzima ya kilimo.
Ufanisi katika manunuzi ya pembejeo, uzalishaji na pia matumizi ya
teknolojia za kisasa (mbegu, mbolea na hata vitendea kazi-mashine) na
hata ufanisi katika kutafuta masoko ya mazao yao mojakwa moja," alisema
Westhuizen.
Chanzo: Michuzi blog