Wizara zaungana ili kupata nguvu ya pamoja ya kutekeleza programu ya kitaifa ya kupanda miti

Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Mungano, Bw. January Makamba (kulia) akifafanua jambo wakati alipokutana na Waziri wa Malias... thumbnail 1 summary
Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Mungano, Bw. January Makamba (kulia) akifafanua jambo wakati alipokutana na Waziri wa Maliasili na Utalii,Profesa Jumanne Maghembe (wa tatu kushoto) makao makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii jinini Dar es Salaam. (Pili kushoto) ni aliyekuwa  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt.Adelhelm Meru, na kulia ni Naibu Katibu Mkuu,Bw. Selestine Gesimba
Programu ya kitaifa ya kupanda na kutunza mazingira inaanza mwezi Januari 2016, hii ni kwa mujibu wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe.
 
Akizungumza katika kikao cha pamoja na Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Mungano, Bw. January Makamba, Waziri Maghembe alieleza kuwa Tanzania imetenga maeneo makubwa ya hifadhi ya misitu na mazingira ili kuhifadhi na kuongeza kuwango cha maji nchini. 
Profesa Maghembe ambaye katika serikali iliyopita alikuwa waziri wa maji, alieleza umuhimu wa miti na misitu katika kuhifadhi maji na umuhimu wa maji kwa viumbe hai.
"maeneo makubwa haya ya hifadhi ya misitu na mazingira yametengwa ili yasaidie kupata hewa nzuri kwa afya yetu, maji, mvua, kuzuia joto kupanda na kupambana na mabiliko ya tabianchi yanayotishia nchi kugeuka jangwa.” anasema Maghembe
Anasema kumekuwa na ukataji mkubwa wa miti na uharibifu wa mazingira nchini na kueleza kwamba programu hii itakayoanza mwezi huu inalenga kuwa na mazingira bora (ecosystem), upandaji miti na utunzaji wake. 
Waziri amesema kikao cha mawaziri husika cha kuweka mkakati wa kutekeleza kampeni hiyo ya upandaji miti na utunzaji mazingira cha siku mbili kitaanza tarehe 16 January na wataalam wa wizara mbili husika tayari wameagiza kuandaa kwa pamoja mkakati utakaotumika kutekeleza programu hiyo. Mkutano wa pamoja utazingatia masuala yote ya upatikanaji wa rasirimali zitokanazo na faida ya misitu na mazingira.
Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira na Muungano,Bw. January Makamba anasema suala la mazingira linagusa shughuli za wizara zote na taasisi nyingi na sekta binafsi na kueleza kuwa kuna kila sababu ya vyombo mbali mbali kushirikiana.  
Amesema programu hii ya kitaifa ni ya aina yake nchini na katika utaratibu huu TAMISEMI itawashirikisha wananchi ili kila mwananchi ajivumie kupanda miti katika eneo lake. 
“Tukitekeleza programu hii kwa uangalifu na kufanikiwa matunda yake yatavutia watu wote wa ndani na nje ya nchi kwa faiada ya taifa letu,” anasema Makamba.