Kampuni
ya simu mkononi ya Airtel kupitia mradi wake wa kusaidia jamii wa
Airtel FURSA imekabidhi vifaa mbalimbali vya ufundi vyenye thamani ya
shilingi milioni 10 kwa mjasiliamali Amina Iddi wa kijiji cha Magole
mtaa wa Chabwanga-Magole Mkoani Morogoro. Uwezeshaji huo kupitia Airtel
FURSA ni kwa ajili ya kutengeneza majiko sanifu maarufu kama jiko matawi
ili kusaidia pia kutunza mazingira ya kijiji hicho na mkoa kwa ujumla .
Kijiji
cha Magole mkoani Morogoro kinakadiriwa kuwa na takribani wakazi kati
ya 1500 na zaidi ambapo shughuli zao kubwa za uchumi ni kilimo cha mazao
ya chakula kama Mahindi, Maharagwe na Mpunga.
Mama
mzazi wa Amina Iddi, Asia Juma (50)alieleza kufurahishwa na kitendo cha
mwanae kupata msaada huo wa vifaa na malighafi zake kwa ajili ya majiko
hayo yenye kubana matumizi na rafiki kwa mazingira.Majiko matawi yana
uwezo wa kutumia mkaa na kuni chache huku yakiwa na sifa ya kuhifadhi
joto kwa muda mrefu sambamba na kutoa moshi mchache.
Tunashukuru
kwa msaada huu wa vifaa vitakavyomwezesha Amina kuendelea na shughuli
zake za ujasiliamali, Amina anabidii na jitihada za hata kutoa ujuzi kwa
vijana wenzie . Wingi wa majiko matawi itasaidia kuokoa mazingiza ya
kijiji.
Kwa
upande wake Bi, Amina Iddi (20) baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo
alieleza kufurahishwa na mpango wa kampuni ya Airtel kupitia Airtel
FURSA kwa jitiada zake za kuwawezesha vijana wajasiriamali katika nyanja
mbalimbali za kuzalishaji mali.
“ndoto
yangu sasa imetimia baada ya kupata vifaa hivi, vitaniongezea
uzalishaji na utengenezaji wa majiko sanifu na kunipa chachu ya kuwa
mbunifu zaidi. Sasa nina uwezo wa kutengeneza majiko sanifu kati ya 10
hadi 15 kwa siku, kabla ya hapo manunuzi ya vifaa hivi, yalinikwamisha
na gharama zilikua juu jiko moja lilikuwa linagharimu kiasi cha sh14,000
baada ya kununua vipuli na kuuza kwa wateja kati ya sh18,000 hadi sh
25,000 lakini kwa sasa baada ya kupata vifaa hivi vitasaidia kuondokana
na gharama za pesa za kununua vifaa, pia nitayauza kwa bei nafuu kwa
wakazi wa hapa kijijini”.alisema Amina.
Meneja
wa Mradi wa jamii wa Airtel Fursa Bi, Hawa Bayumi alisema kuwa “Airtel
FURSA imelenga kuwawezesha vijana wajasiliamali wenye malengo ya ubunifu
kama Amina leo ili kukuza biashara zao na kuleta ubunifu kwa faida ya
jamii nzima.
Bayumi
alieleza “Airtel FURSA mwaka huu ipo katika msimu wa pili na imetenga
jumla ya bilioni 1 kwaajili ya wajasiliamali nchi nzima, ndani ya mizezi
mitatu tayari imeshawaguza vijana 600 kwa kuwapatia elimu ya
ujasiliamali na wengine 14 kufaidika na msaada wa vifaa vya kutendea
kazi ambapo mkoa wa Morogoro umefaidika kupitia kuwezesha kwa
wajasiliamali, Amina Iddy (20) kutoka kijiji cha Magole wilaya ya Kilosa
na Hashimu Mikidadi wa halmashauri ya wilaya ya Morogoro vijijini.
“Tunajivunia
vijana wa Mkoa wa Morogoro waliooonyesha uthubutu kama Amina na Hashimu
ambaye yeye alipata fedha zilizotumika katika ukarabati wa bucha ya
nyama na vifaa ikiwemo majokofu ya kuhifadhia nyama ikiwa na thamani ya
sh9 Mil wakati Amina amepatiwa vifaa vya kutengeneza majiko safuni
vyenye thamani ya sh10 Mil”.alisema Bayumi.
Mjasiliamali
Amina Iddi (20) (kulia ) akijaribu moja ya vifaa alivyokabidhiwa na
Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa wa kuwezesha vijana wenye
umri wa miaka 18 hadi 24 akizungusha mashine ya kutengenezea majiko
sanifu baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo vyenye thamani ya sh10 Mil
kijijini kwao Magole mtaa wa Chabwanga wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro
jana.
Meneja
huduma kwa jamii Hawa Bayumi akimkabidhi kijana Amina Iddi (20) sehemu
ya vifaa vya kutengenezea majiko sanifu vyenye thamani ya sh 10 Mil
baada ya kuwezeshwa na mpango wa Airtel Fursa katika hafla iliyofanyika
nyumbani kwao katika kijiji cha Magole mtaa wa Chabwanga wilaya ya
Kilosa mkoani Morogoro. Kulia ni mama wa Amina, Asia Juma (50) na
kushoto ni afisa mauzo wa Airtel Aminata Keita.
Meneja
huduma kwa jamii Hawa Bayumi akionyesha moja ya jiko sanifu ambalo
bado halijakamili yanayoandaliwa na mjasiliamali Amina Iddi (20)wa tatu
kulia baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa
katika hafla iliyofanyika nyumbani kwao katika kijiji cha Magole mtaa
wa Chabwanga wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.
Chanzo: Michuziblog