Huu ni wakati wa wasanii wa filamu na muziki kuvitumia vivutio vya
Taifa katika kazi zao baada ya Meneja wa mawasiliano wa Hifadhi za Taifa
(Tanapa), Pascal Shelutete, kuwataka wasanii wa filamu nchini kutumia
mandhari za asili zilizoko katika hifadhi za Taifa kwa ajili ya kurekodi
filamu zao ili kutangaza utalii wa ndani.
Shelutete alisema hayo katika tamasha la chama cha wasanii wa filamu
wa jijini Arusha (TFDAA) katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, akidai
kwamba Tanapa itatoa ushirikiano kwa wasanii watakaoonyesha nia ya
kurekodi filamu zao katika maeneo ya hifadhi ambayo ni salama na yenye
mvuto mkubwa.
“Nchi yetu imejaliwa vivutio vingi hivyo wasanii washirikiane na
Tanapa kuutambulisha utalii wetu ili ziweze kuchangia pato la Taifa,”
Shelutete aliliambia gazeti la Mtanzania
Naye Rais wa Shirikisho la Silamu nchini (TAFF), Simon Mwakifamba,
aliwataka wasanii watumie fursa ya maonyesho ya kimataifa ya filamu
yanayojulikana kama Tanzanite International Film Festival
yatakayojumuisha wasanii wa filamu kutoka nchi mbalimbali duniani
kujitangaza na kutengeneza marafiki wakusaidiana katika sanaa zao.