Wanafunzi wasiopanda miti kunyimwa vyeti Iringa

Sharti pekee la mwanafunzi kupata cheti cha kuhitimu elimu ya msingi na sekondari nchini lilikuwa kuhudhuria shuleni, kufanya mitihani na ... thumbnail 1 summary
Sharti pekee la mwanafunzi kupata cheti cha kuhitimu elimu ya msingi na sekondari nchini lilikuwa kuhudhuria shuleni, kufanya mitihani na kufaulu, lakini sasa limeongezwa la kupanda miti ambalo halina uhusiano na masomo darasani. planting-trees
Kuanzia mwakani, moja ya masharti ya mwanafunzi kupewa cheti cha kuhitimu elimu ni kuukabidhi uongozi wa shule mti alioupanda siku ya kwanza alipoanza masomo na akautunza kipindi chote cha masomo.

Sharti hilo lilitangazwa jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba aliposhiriki mpango wa upandaji miti na wanafunzi katika Shule ya Msingi Mlandege iliyopo Kata ya Kwakilosa, Manispaa ya Iringa akiongozana na viongozi wa mkoa.
Source: Mwananchi