Shirika la Kuhifadhi Misitu ya
Asili Tanzania (TFCG) kwa kushirikiana na MJUMITA chini ya ufadhili wa Serikali
ya Uswisi (SDC), wamewajengea uwezo wananchi katika vijiji vinavyotekeleza
miradi ya Usimamizi Shirikishi ya Misitu na Matumizi Endelevu wa mazao
yanayotokana na misitu juu ya umuhimu wa kushirikisha makundi yote katika jamii
katika kuhifadhi na matumizi ya rasilimali zinazotokana na sekta hiyo kwa manufaa
ya jamii.