POLISI WACHOMA MOTO NYUMBA 90 ZA RAIA WILAYANI MAGU, WAONGOZWA NA MKUU WA WILAYA

Hali halisi. KAYA    55 Wilayani Magu, mkoa wa Mwanza hazina mahali pa kuishi baada ya nyumba zao zaidi ya 90 kubomolewa kisha k... thumbnail 1 summary
Hali halisi.

KAYA  55 Wilayani Magu, mkoa wa Mwanza hazina mahali pa kuishi baada ya nyumba zao zaidi ya 90 kubomolewa kisha kuchomwa moto ikiwa ni sehemu ya kutimiza amri ya serikali za kuwaondoa wananchi wa eneo hilo linalotajwa kuwa ni hifadhi ya taifa.
Tukio hilo la kinyama linadaiwa kufanyika kuanzia tarehe 1 Agosti hadi Agosti 2 mwaka huu, ambapo zoezi hilo liliendeshwa chini ya usimamizi wa mkuu mpya wa wilaya hiyo Jaquline Liana akishirikiana na jeshi la  polisi wilayani humo.

Wakizungumza na g sengo blog kuhusiana na tukio hilo, wananchi hao wameilaumu serikali kwa kusema kuwa imeonesha ukatili wa hali ya juu kwa kuwavunjia nyumba zao,  ili hali wakijua kabisa hawana uwezo hata wa kujenga mabanda kwa mifugo iwe vipi ndani ya muda wa wiki mbili wawe na mtaji kujenga nyumba za kuishi?.. hakika ni kitendo ambacho kinakiuka haki za binadamu na utawala bora.
Wamesema kuwa askari hao walitumia silaha za jadi kuvunja na kuchoma moto nyumba zao.

Moja kati ya waliovunjiwa na kuchomewa nyumba zao Bw. Paulo nkiligila akiwa na familia yake asijue wapi pa kujisitiri, zaidi ya kuishi chini ya minyaa
Ilielezwa kuwa kuvunjwa kwa nyumba hizo za vijiji vya Mwabulenga, Misungwi,Bugalu  na Salama ni sehemu ya mikakati ya serikali kutaka kugeuza eneo hilo la Sayaka kuwa  hifadhi ya taifa, ambayo wananchi hao wanadai wamekuwapo zaidi ya  miaka 70 tangu enzi za babu zao.



Pichani ni Emmanuel James Salala ambaye ni Mjumbe wa Serikali ya kijiji.
Mmoja wa wathirika wa tukio hilo, Manhe Mayoka (80) alisema ameishi hapo akirejea nja ya mwaka 1940 anashangaa leo eneo hilo wanaambiwa wapishe ni hifadhi ya taifa, mzee huyo amevunjiwa nyumba zake tatu.

Moja kati ya familia zilizo athiriwa na bomoa na nyumba zao kuchomwa moto kutoka kushoto Kija Mahenhe, Rebeca Mahenhe, Maria Mahenhe, Mariam Manhungwa na mtoto aliyebebwa ni Clement. Familia hii imejisitiri pembezoni mwa kuta za mwenyekiti wa kitongoji cha Itongo kijiji cha Bugatu wilayani Magu Bw. Kulwa Ezekiel  
Wananchi walioathiriwa na kadhia hiyo ni wa vijiji vya Misungwi Kata ya Sukuma na katika kata ya   Ng’aya ni , Mwabulenga, Salama  na Bugatu  wilayani Magu na baadhi ya vijiji vya wilaya ya busega.

Hii ndiyo himaya wa mwenyekiti wa kitongoji cha Itongo kijiji cha Bugatu wilayani Magu Bw. Kulwa Ezekiel 

Haya ndiyo maisha ya wananchi hawa waliovunjiwa nyumba zao kisha kuchomewa, wamekusanya baadhi ya makuti ya nyumba yao ya zamani na  matofali kisha wakatengeneza kingo na hapo ndipo wanapolala. 

Huyu na familia yake ameamua kuhama la faa lake la kuhifadhia chakula akijihifadhi pembezoni mwa nyumba ya mwenyekiti kusubiri ujenzi wa nyumba yake mpya ambao hata hivyo hajajuwa wapi pa kujenga na atajengaje ile hali hakupata hata fidia kama mtaji wa ujenzi.

Pa kujisitiri familia 

Licha ya kutokujua hatma ya pa kulala vijana hawa kamera yako iliwanasa wakijisomea kulia ni Ndutu Samson (20) anayesoma kidato cha 4 na Bukong'one Zacharia (16) anayesoma kidato cha 3, wote katika Shule ya sekondari Ng'aya wilayani Magu. 


Hapa palikuwa bafu.. si waona jiwe la kujisugulia?

Hali tete....

Wamevunja nyumba zooooote za kizungu lakini hiki kijumba wamekibakiza ... "Au ni Yale mambo ya Vunja Uone?"
by G. Sengo

Ni familia ya watoto watano ya Bi. Sabina Joseph katika makazi mapya.

Naye huyu akiwa na mwanaye na mumewe hayuko pichani ambao wanatajwa kuwa walifunga harusi hivi karibuni tu na kupata mtoto huyo kilichofuata nyumba ikabomolewa na kuchomwa na sasa wanajisitiri pembezoni mwa kuta za mwenyekiti wao wakisubiri siku isiyofahamika kuishi maisha kama ya awali yaani ndani ya nyumba. 

Mama akihangaika na pichi jiko la nje.

Batinde Nyaruge mmoja kati ya waliovunjiwa nyumba