Ukosefu wa wakufunzi, vifaa vya kujifunzia vyachangia uhaba wataalamu wa sayansi ya nyukilia barani Afrika

Changamoto za uhaba wa wakufunzi wa masuala ya nyuklia sambamba na vifaa kwa ajili ya mafunzo hayo barani Afrika vinatajwa kuwa kikwazo kat... thumbnail 1 summary
Changamoto za uhaba wa wakufunzi wa masuala ya nyuklia sambamba na vifaa kwa ajili ya mafunzo hayo barani Afrika vinatajwa kuwa kikwazo katika kuwaandaa wataalamu wa sayansi ya nyuklia hali inayochangia ukosefu mkubwa wa wataalamu hao.
Njia ya elimu kwa mtandao yaan E-learning inatajwa kama moja ya njia zitakazosaidia uboreshwaji wa utoaji wa mafunzo hayo katika vyuo vikuu barani Afrika, lakini changamoto kubwa iliyopo ni uhaba wa wakufunzi wa sayansi ya nyuklia na vifaa vinavyohitajika katika mafunzo.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa ambaye licha ya kusisitiza umuhimu wa njia hiyo pia anasema serikali ya Tanzania inafanya jitihada kubwa za kuhakikisha inatengeneza mazingira yatakayorahisisha njia za mafunzo, akitolea mfano wa ujenzi wa mkongo wa taifa ambao umerahisha kwa kiasi kikubwa huduma za mawasaliano hivyo kuwezesha mafunzo kwa njia ya mtandao kufanyika nchini.
Mkurugenzi wa tume ya mionzi Tanzania Profesa Juma Mkilaha amesema mkutano huu una lengo kuu la kujadili mkakati maalumu utakaoelekeza namna vyuo vitakavyoshirikiana katika kutoa mafunzo ya sayansi ya nyuklia ikiwa ni pamoja na kubadilishana wakufunzi.
Nae Mwenyekiti wa AFRA-NEST Profesa Shaukat Abdulrazak amesisitiza kuwa ili nchi za afrika ziweze kupiga  hatua katika sekta ya Nyuklia hazina budi kutia mkazo katika masomo ya sayansi sambamba na kuboresha miundombinu.

Mkutano huo wenye lengo la kujadili namna ya kuboresha utoaji wa elimu ya sayansi ya Nyuklia katika vyuo vinavyotoa mafunzo hayo ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa wataalamu wa nyuklia katika nchi za Afrika, unawakautanisha wataalamu mbalimbali kutoka katika sekta za nyuklia na vyuo vikuu vinavyotoa mafunzo ya sayansi ya nyuklia kutoka katika nchi zipatazo 31 ambazo  ni wanachama wa umoja huo.