Fuvu la Mkwawa lawa kivutio kikubwa cha utalii

 Fuvu la aliyekuwa chifu wa kabila la Wahehe mkoani Iringa ambaye alijiuwa kwa kukataa mwili wake kuguswa na wajerumani enzi ya Ukolon... thumbnail 1 summary
 Fuvu la aliyekuwa chifu wa kabila la Wahehe mkoani Iringa ambaye alijiuwa kwa kukataa mwili wake kuguswa na wajerumani enzi ya Ukoloni, kwa sasa limehifadhiwa katika himaya yake kama moja ya  kumbukumbu muhimu za Taifa.

 Balozi wa amani nchini Risasi Mwaulanga akiwa na vifaa vilivyotengenezwa kiasili katika eneo hilo la makumbusho kalenga mkoani iringa


 moja ya kaburi lililopo katika eneo hilo ambalo li la mwanafamilia wa Mkwawa.

 Hili ni jengo ambalo ndani ndipo walipohifadhi fuvu hilo na baadhi ya vitu vya asili ya wahehe ambavyo hutumiwa na machifu.

kwa mtu yeyote aliyesoma historia, jina la Chifu Mkwawa halitakuwa geni masikioni mwake na kwamba kumbuku hiyo ni muhimu kwa vizazi hadi vizazi.
Ikumbukwe kwamba katika chumba hicho kilichohifadhi fuvu halisi la Mkwawa kwa sasa hutumika kama moja ya makumbusho ya kitaifa na hivyo kila aliyetaka kufika hapo kwaajili ya kuangalia kwa uhalisia fuvu hilo ni lazima alipie kiasi cha shilingi 1000 kwa mtu mmoja na kwamba fehda hizo zinzdaiwa kuwa ni sehemu ya kufanya matumizi ya utunzaji wa mandari hiyo.

Ama hakika kwa kuangalia kialisia kwa waliofanikiwa kufika katika eneo hilo mazingira yake yanavutia na kwamba kwa mtazamo wa haraka haraka kwa nje utadhani nyumba hiyo ni ya kuishi watu.