Maporomoka yahofiwa kuuwa wengi

  Shirika la msalaba mwekundu nchini Uganda limesema kuwa zaidi ya watu kumi na wanane wamefariki dunia katika maporomoko hayo. ... thumbnail 1 summary

 



Shirika la msalaba mwekundu nchini Uganda limesema kuwa zaidi ya watu kumi na wanane wamefariki dunia katika maporomoko hayo.

Zaidi ya nyumba kumi na tano zimezikwa kufuatia mvua kubwa iliyonyesha katika eneo hilo.

Shirika hilo limesema maafisa wake wanaendelea kuwatibu waliojeruhiwa katika mkasa huo, katika eneo hilo lenye rutuba la Bududa, linalokuza kahawa na lililopo karibu na mbuga ya wanyama ya mlima Elgon.
Bududa, Uganda

nyumba zimefunikwa futi16 chini

Mwandishi wa habari, Stephene Mulaa, aliyezuru eneo la tukio amesema kuwa, ''kufikia jana jioni hakuna mwili hata mmoja ulikuwa umepatikana, kwa sababu inakadiriwa kwamba miili ya watu na nyumba zilizofunikwa na udongo ziko zaidi ya futi kumi na sita kwenda chini''

serikali kuwasaidia walioathirika

Serikali ya Uganda inatarajiwa kutoa taarifa kamili kuhusu janga hilo baadaye hivi leo.
Lakini kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, serikali imesema kuwa,'' inafanya juu chini kuhakikisha kuwa familia zilizoathirika zinapata msaada wa kutosha''.
Waziri anayehusika na maswala ya majanga, Dr Steven Malinga, amenukuliwa katika taarifa akisema kuwa hakuna madhara makubwa yaliyoripotiwa.
Mwaka 2010, maporomoko mengine ya ardhi yalitokea katika wilaya hiyo ya Bududa, na kuwauza zaidi ya watu mia tatu.
Eneo hilo linazungukwa na miinuko pamoja na mabonde, kando kando ya mlima Elgon, na hupokea mvua kubwa katika msimu wa masika.
Serikali imewashauri wakazi katika maeneo hayo kuhamia maeneo salama lakini wengi wamekataa kufanya hivyo wakihofia kupoteza mashamba yao yenye rotuba.