Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameombwa
kuiga mfano wa Wabunge wa Zimbabwe kwa kujitokeza kutahiriwa ikiwa ni hatua
moja wapo ya kupambana ana maambukizi ya virusi vya Ukimwi nchini.
Wito huo umetolewa leo Bungeni Mjini Dodoma na
Mbunge wa Konde (CUF) Khatib Haji ambapo alisema kuwa mfano huo ni wa kuigwa na
Wabunge wote ambao hawajatahiria wanapaswa kufanya hivyo ili kuwahamasisha wananchi
wao.
Wiki iliyopita Wabunge nchini
Zimbabwe wametahiriwa kama moja wapo ya hatua zao ya kukabiliana na kusambaa
kwa virisi vya Ukimwi nchini humo
Njee ya majengo ya bunge mjini Harare ,
kulijengwa zahanati ndogo kwa sababu ya shuhuli hizo za kuwapasha wabunge
tohara.Blessing Chebundo, ambaye ni mwenyekiti wa wabunge wanaopambana na Ukimwi amesema nia yake hasa ya yeye kuamua kupashwa tohara ni kuchochea wanaume nchini Zimbabwe kutairiwa.