Mussa Mwangoka, Sumbawanga.
WAKAZI wa mkoa wa Rukwa wametahadharishwa juu ya utunzaji wa chakula kwa kuwa upo uwezekano mkubwa wa baadhi ya maeneo ya mkoa huo kukabiliwa baa la njaa kutokana na uzalishaji mazao hayo kutokuwa mzuri kama ilivyotarajiwa.
Mratibu wa asasi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na utunzaji wa mazingira ya Kaengesa Environmental Conservation Society (Kaeso) iliyopo wilaya ya Sumbawanga, Joel Amon, alitoa tahadhari hiyo jana wakati akizungumza na mwandishi wa habari ofisi kwake kuhusu athari zilizojitokeza kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
Alisema Kuwa hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula hususani mahindi katika wilaya za Sumbawanga na Nkasi si wakuridhisha ukilinganisha na misimu mingine ya kilimo hali iliyojitokeza kutokana na mabadiliko ya tabia nchi yaliyosababishwa na uharibifu wa mazingira.
WAKAZI wa mkoa wa Rukwa wametahadharishwa juu ya utunzaji wa chakula kwa kuwa upo uwezekano mkubwa wa baadhi ya maeneo ya mkoa huo kukabiliwa baa la njaa kutokana na uzalishaji mazao hayo kutokuwa mzuri kama ilivyotarajiwa.
Mratibu wa asasi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na utunzaji wa mazingira ya Kaengesa Environmental Conservation Society (Kaeso) iliyopo wilaya ya Sumbawanga, Joel Amon, alitoa tahadhari hiyo jana wakati akizungumza na mwandishi wa habari ofisi kwake kuhusu athari zilizojitokeza kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
Alisema Kuwa hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula hususani mahindi katika wilaya za Sumbawanga na Nkasi si wakuridhisha ukilinganisha na misimu mingine ya kilimo hali iliyojitokeza kutokana na mabadiliko ya tabia nchi yaliyosababishwa na uharibifu wa mazingira.
"yapo maeneo katika mkoa huu kumejitokeza ukame kwa kuwa mvua
hazijanyesha lakini yale ambayo mvua zimenyesha si kwa kipindi ambacho
wakulima walitegemea, kuna sehemu mvua ziliwahi isivyo kawaida na
zikakatika mapema sana...... sasa hii iliathiri kwa namna moja au
nyingine” alisema.
Pia alisema kuwa tatizo jingine lililosababisha kuwepo kwa hali hiyo ni uchakachuaji na udanganyifu mkubwa uliojitokeza katika zoezi la usambazaji wa pembejeo za kilimo kupitia mfumo wa vocha.
Alisema kuwa ni vizuri wakulima wakaweka akiba ya chakula si kukiiza chote kama ilivyo kawaida kwani kutokana na uzalishaji kuwa wa chini ukilinganisha na msimu mingine, pia mavuno yanatarajia kuwa kidogo na hali itakuwa mbaya miezi michache ijayo".
Kwa mujibu wa takwimu za kilimo, zinaonyesha kuwa kwa msimu wa kilimo wa 2010 hadi 2011 ulizalisha ulikuwa tani 2,136,345 za mazao ya chakula huku msimu ujao wa mavuno wanategemea kuvuna 2,518,270 za mazao cha chakula ambazo huenda zisifikiwe.
Pia alisema kuwa tatizo jingine lililosababisha kuwepo kwa hali hiyo ni uchakachuaji na udanganyifu mkubwa uliojitokeza katika zoezi la usambazaji wa pembejeo za kilimo kupitia mfumo wa vocha.
Alisema kuwa ni vizuri wakulima wakaweka akiba ya chakula si kukiiza chote kama ilivyo kawaida kwani kutokana na uzalishaji kuwa wa chini ukilinganisha na msimu mingine, pia mavuno yanatarajia kuwa kidogo na hali itakuwa mbaya miezi michache ijayo".
Kwa mujibu wa takwimu za kilimo, zinaonyesha kuwa kwa msimu wa kilimo wa 2010 hadi 2011 ulizalisha ulikuwa tani 2,136,345 za mazao ya chakula huku msimu ujao wa mavuno wanategemea kuvuna 2,518,270 za mazao cha chakula ambazo huenda zisifikiwe.
Mwisho.