Umuhimu wa mazingira kwa uchumi wa Tanzania uko katika sura nne zifuatazo

  ¨       Mazingira yanaipatia nchi mahitaji yote ya msingi kwa ajili ya kufanikisha masuala ya jamii na uchumi. ¨       Mazingira n... thumbnail 1 summary

 ¨      Mazingira yanaipatia nchi mahitaji yote ya msingi kwa ajili ya kufanikisha masuala ya jamii na uchumi.
¨      Mazingira ndiyo makazi ya viumbe vyote – memea na wanyama ambao ndiyo urithi usiokuwa na badala yake.
¨      Mazingira ni chombo cha kuweka yale yasiyofaa.
¨      Mazingira ni msingi ambao ndiyo itakuwa jawabu la kupunguza unyonge wa umaskini.

Kwa hiyo ni dhahiri kwamba msukumo mkubwa wa uongozi wa mazingira ni kulinda sehemu asili ya kuishi binadamu na kuoanisha upungufu uliopo kwenye mazingira katika kusaidia kufikia maamuzi yanayohusu masuala na shughuli za uchumi.
Serikali ya Tanzania ilitambua hatari ya kupoteza rasilimali hiyo kama vile hewa safi, mabaki ya mimea na wanyama wa kale, nyangumi, miti ya asili na wanyama/mimea ambayo iko mbioni kutoweka.
Katika kurekebisha hali hiyo, serikali imechukua hatua thabiti kwa kutengeneza sera, sheria na mfumo wa taratibu ambazo zinaendana na masuala ya jamii, uchumi na siasa.
Serikali kwa kushirikiana na washika dau mbalimbali wameweka mkazo katika kuendeleza kukuza na kuhamasisha ushirikishwaji wa jumuiya na watu binafsi katika kuimarisha uhifadhi na uongozi wa mazingira.  Pamoja na hayo kulikuwa na kampeni za kutambua umuhimu wa mazingira, elimu ya mazingira na kuendeleza ujuzi ambao ulisaidia katika kuhifadhi na kuendesha masuala ya  mazingira.  Mkazo wa kuhifadhi na kusimamia mazingira ni kwa ajili ya kukuza uwezo na akili za jamii na watu binafsi katika kudumisha usimamizi kwa manufaa yao na manufaa ya vizazi vijavyo. Inatia moyo kwamba juhudi hizo zimeamsha fahamu za watu, moyo wa kupenda na  vitendo vya kusaidia kwa sababu zaidi ya idadi 159 ya CBO’s (Community Based Organiations) na NGO’S (Non-Governmental Organisations) zimeundwa zikiwemo pia na sekta binafsi na watu binafsi kujiunga katika mkumbo.  Isitoshe, Serikali kwa kushirikiana na mashirika na mawakala kama vile CBO’s/NGO’s wanatekeleza mipango mbalimbali katika maeneo ya mijini na vijijini.  Vyombo vya habari (radio, televisheni, magazeti) vimefanyaka kazi nzuri katika kuhamasisha na  kutangaza vipindi mbalimbali vya elimu kuhusu masuala ya mazingira na hivyo kutoa mafunzo kwa hadhara na watu binafsi ya kuwa na moyo wa kupenda, kujituma na kufahamu jinsi ya kuhifadhi na kusimamia mazingira.
Serikali ilitumia sera za sekta zinazohusiana na misitu, madini, wanyama pori, samaki, kilimo, mifugo na ardhi ambazo zimeweka kipaumbele masuala ya usimamizi na hifadhi za rasilimali na mazingira, kukuza kufahamu wa wananchi wa kuelewa uhusiano kati ya mazingira na uhai na kuendeleza ushirikiano wa kimataifa kuhusu ajenda ya mazingira.
Ni dhahiri kwamba uhifadhi na usimamizi wa mazingira duniani na kitaifa una nia ya kushinda matatizo yanayotokana na umaskini, maradhi, hali mbaya na duni ya upatikanaji wa chakula, makazi machafu, maji yasiyo salama, upatikananji wa nishati usioridhisha na ukosefu wa ajira.
 
Kuelewa kwa wananchi na watu binafsi juu ya faida za kuhifadhi na kusimamia mazingira ndiyo msingi wa kuendeleza rasilimali na mazingira.  Hiyo inakwenda sambamba na utekelezaji wa mipango thabiti ya kuondoa umaskini kwa sababu umaskini unaendana na matumizi mabaya ya rasilimali na uharibifu wa mazingira na hivyo juhudi za kuuondoa umaskini zinahitaji ushirikiano wa jinsia zote.  Zaidi ya hayo, serikali imeamua kushughulikia hifadhi na usimamizi wa mazingira pamoja na kuondoa umaskini ukishirikiana kikamilifu na watu binafsi, CBO’s, NGO’s na wafadhili.