Polisi Katavi wakamata Nyara za mamilioni ya fedha

Mussa Mwangoka, Katavi   POLISI  wilayani  Mpanda  katika mkoa  wa  Katavi  inawashikilia  watu  10 miongoni  mwao  wakiwemo  wanawa... thumbnail 1 summary

Mussa Mwangoka, Katavi
 
POLISI  wilayani  Mpanda  katika mkoa  wa  Katavi  inawashikilia  watu  10 miongoni  mwao  wakiwemo  wanawake  wawili   kwa tuhuma ya kukamatwa na nyara za Serikali  zenye  thamani  ya  zaidi  ya Sh  milioni 80  kinyume  cha  Sheria .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ,  Dhahiri Kidavashari alisema kuwa  watuhumiwa hao  waliokamatwa katika  matukio  tofauti   wilayani   humo  kufuatia  msako  mkali  ulioshirikisha Jeshi  la Polisi,  askari  wanyamapori   kutoka  Tanapa  na Hifadhi ya Taifa ya  Katavi .

Alidai  kuwa  pamoja  na   kuwakamata  watuhumiwa  hao  katika  msako  huo pia    timu   hiyo  ya askari  ilikamata  meno  ya  tembo  matano  yenye thamani  ya zaidi ya Sh milioni  73  nyama  ya  nyati  yenye  thamani ya zaidi ya Sh  milioni 7.2.

Pia  misumeno 5 , mizani  miwili ,  mabegi  manne  na magari  mawili  aina  ya Noah  yalikamatwa  kufuatia msako  huo, ambapo katika tukio  la  watuhumiwa  watano  walikamatwa  katika kijiji  cha Msaginya  wilyani  humo  katika  Barabara  ya Mpanda – Tabora  wakiwa na  meno  ya tembo  matatu  yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 50 kinyume cha  sheria.

Aliwataja  watuhumiwa  hao  kuwa ni pamoja na  Joseph  Mahundi  maarufu kama  Ngondo (59), makzi  wa Kigoma , Msafiri Nyirawi  (36) na Abubakari  Mhina  (25)  ambaye ni   dereva  wote   wakiwa  wakazi  wa mjini  Dodoma .

Wengine  ni pamoja na Peter Mashihamvula (55) mkazi  wa  kitongoji  cha  Kawajense  mjini  Mpanda  na David Simwanza  (38)  mkazi  wa  kijiji  cha Lwasho  wilyani Mbozi   katika mkoa  jirani  wa  Mbeya .

Kwa mujibu  wa  Kamanda  Kidavashari  nyara hizo  za Serikali  zilikamatwa  zikiwa  zinasafirishwa kuelekea   mjini  Dodoma  katika  gari  aina  ya Noah  yenye   namba  za usajiri  T983 TZJ   lililokuwa  likiendeshwa na  Mhina.

Katika  tukio  jingine  lililotokea juzi  saa  kumi  jioni  watu  watatu  wakiwemo  wanawake  wawili  walikamatwa wakiwa na  meno  mawili ya tembo  yenye thamani  ya  zaidi  ya Sh  milioni  24 kinyume  cha sheria.

Aliwataja  watuhumiwa hao  kuwa ni pamoja na  Rose  Bwigilo (36)  mkazi  wa Kimara Mwisho Jijini   Dar Es Salaam , Adelina  Alphonce (39)  mkazi  wa  Tabata   na  John Venance  (26)  akiwa pia mkazi  wa  Jijini  Dar Es Salaam.

Siku  hiyo  ya tukio  kwa mujibu  wa Kamanda Kidavashari watuhumiwa hao  wa likamatwa  na  nyara  hizo  katika  gari  la  aina  ya Noah  yenye  namba  za usajiri  T463 BZW iliyokuwa  ikiendesha na  John  pia  msumeno , na  mizani  vilikamwatwa  vikiwa  vimefichwa ndani  ya gari hilo.

Katika  tukio  jingine watu wawili  walifahamika  kuwa ni Juma Ngeleka  (30)  mkazi  wa kitongoji  cha Kawajense  mjini Mpanda   na John Mlelwa  (25) mkazi  wa Inyonga  wilyani  Mlele  wamekamatwa na  nyama ya  nyati  yenye  thamani  yenye  zaidi  ya  Sh  milioni 7.5.

Kwa mujibu  wa Kamanda  Kidavashari  watuhumiwa  hao  walikamatwa  Juni 28 mwaka  huu  wilayani  humo  ambapo  msako  bado  unaendelea  ili  kuwabaini  watuhumiwa  wengine . 

Mwisho