WATANZANIA WATAKIWA KUPIGIA KURA MLIMA KILIMANJARO, NGORONGORO CRATER NA SERENGETI.

  Mwenyekiti wa Shirikisho la Utalii Tanzania TCT, Gaudence Temu  Na Idd Uwesu, Arusha yetu Watanzania wametakiwa kuyapigia kura... thumbnail 1 summary

 Mwenyekiti wa Shirikisho la Utalii Tanzania TCT, Gaudence Temu 

Na Idd Uwesu, Arusha yetu
Watanzania wametakiwa kuyapigia kura maeneo matatu ya asili ambayo ni moja ya vivutio vikuu vya utalii hapa nchini ili yaweze kushinda na kuwa moja ya maajabu saba ya dunia.
Maeneo hayo ambayo ni Mlima wa Kilimanjiro, Kasoko ya Ngorongoro maarufu kama ngorongoro Crater na Hifadhi ya wanyama ya Serengeti.
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Shirikisho la Utalii Tanzania TCT, Gaudence Temu wakati wa uzinduzi wa ndege mpya aina ya Boeng 787 ya shirika la ndege la Ethiopia katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro.
Mwenyekiti huyo wa Shirikisho la Utalii nchini amesema ni fursa muhimu kwa watanzania wote kushiriki upigaji kura huo ili kuyawezesha maeneo hayo muhimu katika uchumi wa nchi kushinda mashindano hayo yatakayosaidia kutangaza nchi yetu na vivutio vya utalii vilivyopo.
Akirejea Kauli ya Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Khamis Kagasheki, alioutoa wakati akiwasilisha Bungeni Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii ya mwaka 2012/13, kuhusu Watanzania kushiriki ipasavyo kwa kupiga kura kwa njia ya elektronik kwenye shindano la ‘Seven natural wonders, Temu amesema huu ndio wakati muafaka kwa watanzania wote kufanya hivyo.
Akizungumzia ujio wa ndege hiyo ya Boeng 787, Temu amesema ni nafasi nyingine kwa Tanzania kuzidi kupanua wigo wa sekta za  usafiri wa anga na utalii hasa kwa kanda ya kaskazini na kuongeza kuwa anapongeza shirika la Ndege la Ethiopia kwa kutoa nafasi kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro kuwa wa kwanza kutumiwa na ndege hiyo kubwa yenye uwezo wa kubeba abiria wapatao 270.
Amesema ujio wa ndege kubwa kama hiyo ya boeng 787 kutarahisha ujio wa watalii kutoka nje ya nchi na kuongeza idadi ya watoa huduma za usafiri wa nga ambao ni kichocheo kikubwa katika kuendeleza sekta ya utalii nchini.

Picha za vivutio vinavyopigiwa kura ili viwe miongoni mwa maajabu saba ya dunia 
 






Chanzo: Arusha yetu