Watalii kukosa walichokitarajia ni kuporomosha uchumi

ZIPO nchi kadhaa duniani zilizoendelea na kuneemeka kwa kutegemea utalii katika kukuza uchumi wake, ambazo zimekuwa zikisimamia vyema kuul... thumbnail 1 summary
ZIPO nchi kadhaa duniani zilizoendelea na kuneemeka kwa kutegemea utalii katika kukuza uchumi wake, ambazo zimekuwa zikisimamia vyema kuulinda na kuukuza, kwa lengo la kuwafanya watalii wa ndani na nje kuongezeka kila siku.
Tanzania ni moja ya nchi chache duniani ambazo zingeweza kuongeza kasi ya kukuza uchumi wake kutokana na kuwa na vivutio vingi vya utalii, zikiwemo mbuga kubwa na nzuri za wanyama, Mlima Kilimanjaro, mito na mabonde yanayowavutia watalii hususan wa nje kuja kutembelea kwa kulipa fedha za kigeni.
Leo unapozungumzia pato linalochangiwa na sekta ya utalii, utakuwa unazungumzia jambo ambalo halina uhakika kwa kuwa utalii unazidi kuporomoka kila kukicha kutokana na sababu mbalimbali, ambazo pia zinawafanya watalii wengi kusitisha safari zao kutoka makwao kwa gharama kubwa kuja Tanzania.
Utalii ni sekta inayotumika kuingiza fedha nyingi za kigeni, lakini iwe kwa kuwashawishi wageni kuingia kwa wingi na wakutane na kile wanachokitarajia na wakirejea makwao wakasimulie walichokiona ili waliowasimulia wapate hamu ya kuja kutalii.
Hakika utalii wa Tanzania ulijitangaza wenyewe, haukutangazwa kama tunavyoona nchi nyingine zikihangaika kuutangaza utalii wake, ili kuwashawishi watalii kuingia, lakini bila mafanikio.
Leo utalii wa Tanzania umegubikwa na dosari mbalimbali zinazowafanya watalii wasiridhike kwa kiwango kikubwa, kwa maana ya kutokidhi matarajio yao, hasa kwa mtalii ambaye alikuja miaka15 iliyopita, hakika akija leo hatafurahi kwa vile utalii wetu umeporomoka sana.
Soma zaidi 
Una taarifa, picha za usafiri wa anga, mazingira, maliasili na utalii? tutumie kupitia kingkahindi@gmail.com