PONGEZI KWA GAZETI LA TANZANIA DAIMA KWA KUCHAPISHA HABARI ZA MAZINGIRA, MALIASILI NA UTALII

Blog ya tabianchi inalipongeza gazeti la Tanzania Daima kwa kuweka kipaumbele na kuchapisha habari za mazingira, maliasili na utalii. u... thumbnail 1 summary
Blog ya tabianchi inalipongeza gazeti la Tanzania Daima kwa kuweka kipaumbele na kuchapisha habari za mazingira, maliasili na utalii. ujasiri huu wa kutoa nafasi kwa habari za aina hii umekuwa ukifanywa na vyombo vya habari vichache sana na pale chombo fulani kinapoonyesha jitihada hizo mimi kama mdau wa masuala ya mazingira, maliasili na utalii na Mtanzania yeyote yule mwenye mapenzi ya kweli na nchi yake hatuna budi kutoa shukran na pongezi zetu.

Nimekuwa nikifuatilia mara kwa mara magazeti yetu hapa nchini kwa zaidi ya miezi miwili sasa na nimebaini kuwa habari za aina hii hazipewi nafasi ipasavyo pamoja na kwamba zinagusa maslahi ya jamii. 

Kama ilivyokauli mbiu ya tabianchi, vita ya mabadiliko ya tabianchi ni ya kila mmoja, hivyo napongeza na kuhamasisha jamii yote kushiriki katika vita hii ikiwa ni pamoja na kutunza, kuhifadhi, kutangaza na kutembelea hifadhi zetu za taifa na makumbusho ya taifa.

Habari na makala haya hapa chini yote yamechapishwa leo katika gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, 11, 2012
Nyalandu awabomoa TANAPA
Bahi wakataa urani kuchimbwa
Watakaoharibu mazingira Muheza kuchapwa viboko
Watalii kukosa walichokitarajia ni kuporomosha uchumi
Mkuhumi na mkakati wa kupunguza umaskini kwa wananchi
REDD + iungwe mkono kuhifadhi sekta ya misitu, kukuza uchumi wa kijani

Una taarifa, picha za usafiri wa anga, mazingira, maliasili na utalii? tutumie kupitia kingkahindi@gmail.com