Afisa Biashara Mkuu wa fastjet
Richard Bordin, ameeleza kuwa uhaba wa safari za ndege kati ya Dar es Salaam na
Johannesburg unaotokana na kuwepo kwa shirika moja la ndege na kukosekana kwa
ushindani kumesababisha kupanda kwa bei za nauli na kwamba fastjet itaziba
pengo hilo.
“Kuanza kwa safari zetu
kutapunguza gharama hizo za ndege na kuongeza kasi ya wafanyabiashara na watu
wa kawaida kusafiri kati ya Dar es Salaam na Johannesburg kwa shughuli
mbalimbali kwa bei nafuu” anasema Bordin
Ikitumia ndege aina ya Airbus
A319, fastjet itafanya safari zake mara tatu kwa wiki na huenda idadi ya ‘ruti’
hizo ikaongezeka katika siku za usoni kutegemea na wingi wa wasafiri.
Taarifa zaidi zinasema kuwa tiketi
za safari kati ya Dar es Salaam na Johannesburg zitaanza kuuzwa siku ya
Jumatano tarehe 31 Julai mwaka huu ambapo nauli ya chini ni dola 100 za
kimarekani sawa na sh. 160,000 za kitanzania.