WANAKIJIJI WACHANGIA MAJI NA FISI,NI KIJIJI CHA SINGITA,KATA YA USANDA WILAYA YA SHINYANGA VIJIJINI

Wananchi wa kijiji cha Singita kata ya Usanda wilaya ya Shinyanga vijijini mkoani Shinyanga wanakabiliwa na uhaba wa maji safi na sala... thumbnail 1 summary
Wananchi wa kijiji cha Singita kata ya Usanda wilaya ya Shinyanga vijijini mkoani Shinyanga wanakabiliwa na uhaba wa maji safi na salama hali inayowafanya kutumia maji ya mto ambayo pia hutumiwa na wanyama aina ya fisi
Wakizungumza juzi na waandishi wa habari baada ya kutembelea kijiji cha Singita kilichopo katika kata ya Usanda wilaya ya Shinyanga vijijini wananchi hao walisema kwa zaidi ya miaka hamsini hawapati huduma ya maji safi na salama kwani wamekuwa maji ya mto Shimiwi ambayo si salama kwa vile hayafai kunywewa.
Wananchi hao walidai kuwa kwa miaka mingi wamekuwa  maji hayo kwa shughuli mbalimbali kama vile kunywa,kufyatulia matofali , kufuria nguo na maji hayo pia yanatumiwa na  wanyama aina ya fisi.
“Kwa kweli haya maji si salama kwa afya zetu kwani wakati mwingine tumekuwa  tukikuta  fisi wamechezea maji hayo na kuacha vinyesi vyao ndani ya maji”,walisema.
“Kijiji hiki kina vitongoji kumi na  mara kwa mara tumekuwa tukipewa ahadi na viongozi wetu kuwa watatuletea maji hayo lakini mpaka leo hakuna lolote hivyo tumeamua kuishi tu na hali yetu kama tulivyo zoea”,aliongeza Juma Hamis mmoja wa wananchi hao.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho Mohamed Jumanne alisema wananchi wake wamekuwa wakitumia maji ya mto huku wengine wakitumia maji ya kwenye majaruba  wakati wa masika kutokana na maji ya mto kuchafuka na kipindi kwa asilimia kubwa kwa kuchanganyikana na vinyesi vya wanyama fisi pamoja na binadamu ambao hujisaidia vichakani.
Jumanne alisema baadhi ya wananchi wa kijiji hicho kwa asilimia kubwa hutumia maji hayo kwa matumizi ya kunywa bila ya kuyachemsha hali ambayo huhatarisha afya zao kwa kukabiliwa na magonjwa hatari yatokanayo na matumizi ya maji
Afisa afya wa kata ya Usanda katika kijiji cha Singita Chade Musa na Muuguzi wa Zahanati wa kijiji hicho Leticia Anthony walisema ni vigumu kubaini idadi ya wagonjwa wanaotokana na maji hayo machafu kutokana na zahanati hiyo kutokuwa na maabara yenye vipimo hivyo, huku wakidai na wao hutumia maji hayo ingawa huyachemsha.
Diwani wa kata ya Usanda Abeid Ndaji kupitia Chama Cha Mapinduzi alikiri kuwepo kwa tatizo la maji safi na salama katika kijiji hicho ambapo alisema mwaka 2012 serikali iliahidi kuwajengea visima virefu vitatu ili kukidhi mahitaji ya wananchi hao lakini wamekuwa wakilifuatilia  bila ya mafanikio.
Diwani huyo alitumia fursa hiyo kumuomba waziri mwenye dhamana kufika katika kijiji hicho kujionea hali halisi ya wananchi hao jinsi wanavyopopata shida ya maji na kuwatatulia tatizo hilo ambalo limekuwa likiwasumbua kwa kipindi kirefu.
“Tatizo la maji safi na salama katika kijiji hiki limekuwa sugu tangu nianze kuwa kiongozi mwaka 1994 kuwa diwani wa kata ya Usanda wananchi hawa wamekuwa wakipata shida ya maji hayo na nimekuwa nikipiga kelele kwenye baraza la madiwani ndani ya miaka 20 wananchi wapatiwe maji hayo bila ya mafanikio “ alisema Ndaji.