Wanafunzi
wa shule ya sekondari Mnazi Mmoja wakiangalia moja ya mfano wa ndege
wakati walipotembelea katika banda la Mamalaka ya Usafiri wa Anga
Tanzania TCAA, Katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea
katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Afisa
Utwala Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma ya Usafiri wa Anga
Tanzania TCAA,Catherine Morarya akiwaonyesha Wanafunzi wa Shule ya
Sekondari ya
Mnazi Mmoja ya jijini Dar es Salaam redio ya upepo inayotumika kwa
mawasiliano ya anga, wakati walipofika kujifunza maswala ya anga katika
banda la Mamlaka
ya Usafiri wa Anga Tanzania kwenye maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma
yanayoendelea hapa nchini.
Afisa
Habari wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania *TCAA* Faustine Ngongo
akiwaelezea baadhi ya wananchi waliofika katika banda hilo lililopo
kwenye Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja
vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.