Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Zaidi ya majangili
400 wamekamatwa katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi
wakiwa na silaha tano za kivita aina
ya SMG na silaha aina ya G3 pamoja na Risasi
357 katika kipindi cha kuanzia june 2013
hadi june 2014
Hayo yalielezwa hapo
jana na Mkuu
wa Idara ya ulinzi wa Hifadhi
ya Taifa ya Katavi Davis Mushi
wakati akitoa taarifa ya Hifadhi ya
Taifa ya Katavi kwenye kikao cha kamati
ya ushauri ya Wilaya ya Mpanda
kilichofanyika kwenye ukumbi wa Idara ya maji
Mjini hapa
Mushi aliwaeleza wajumbe wa
mkutano huo katika kipindi cha
mwaka 2013 na 2014 wamefanikiwa kukamata
majangili 409 wakiwa na silaha za
kivita bunduki aina ya SMG tano ,G3 Bunduki aina
ya Riffle nane , Shortgun 21
magobore 138 Bastola mbili na
Risasi za SMG 357
Alisema kuwepo
kwa makazi ya wakimbizi ya Katumba na
Mishamo karibu na Hifadhi kumesababisha
wakimbizi wa makazi hayo kujihusisha na
shu\ghuli za ujangili kama njia ya kupatia
kipato chao
Alifafanua kati ya majangili
wanaokamatwa na meno ya tembo baadhi yao huwa
ni wakimbizi wanaotoka kwenye makambi hayo
ya wakimbizi ya Katumba na Mishamo
Alieleza wakimbizi toka
kambi hizo ndio waingizaji wakubwa wa
silaha za kivita kama vile Smg , G3 ,
Sar na Ar 15 ambazo wamekuwa wakizitowa Nchini
kwao na kuzitumia kufanyia ujangili ndani ya
Hifadhi ya Taifa ya Katavi
Mushi alieleza uingizaji
wa silaha nyingi za kivita smg , G3 na
Sar kutoka Kigoma unafanywa na
wafanyabiashara haramu wa mano ya
Tembo unaofanywa ilikurahisisha shughuli za ujangili
Alisema silaha hizo
zinapoingizwa hupewa majangili ili kuwawindia tembo
au hudalisha kwa meno ya tembo na silaha
hari ambayo inapelekea kuzagaa kwa silaha nyingi
za kivita na majangili wengi kwa sasa wamebadilisha
matumizi ya silaha kutoka magobore hadi kuwa
silaha za kisasa si kwa kuwindia tembo tuu hata wanyama
wengine
Alltaja sababu
nyingine zinazochangia ujangili katika hifadhi hiyo
ni kuwepo kwa mapoli mengi yasiyo na ulinzi hivyo
kuwa ni sehemu ya kujifichia kwa majangili na pia wanyama
wengi kutoka hifadhi ya Katavi huwindiwa huko mfano
ni msitu wa Msaginya
Aidha magobole mengi
kumilikiwa kihalali hari hii inafanya watu wengi kumiliki
silaha hizo kwani kibali chake ni shilingi elfu moja ambapo kazi
kubwa ya Magobole hayo ni ujangili wa wanyama na
hasa Tembo
Pia kuwepo kwa silaha zinazomilikiwa
na watu kihalali kama vile bundu za aina
ya Rifle watu hao wanamiliki silaha hizo wamekuwa
wakizikodisha kwa majangili
wa wanyama na hasa Tembo
Vilevile kuanzishwa kwa
kwa vijiji kando kando ya Hifadhi na hasa ndani
ya mita 500 toka mpakani mwa hifadhi kinyume cha
sheria ya wanyama pori ya mwaka 2002 hali hii
inapelekea baadhi ya waalifu kuhamia kwenye vijiji
hivyo na kuendesha shughuli za ujangili ndani ya Hifadhi ya
Katavi