RoadToParis2015 with tabianchiblog&CFIMedias21
SIASA!
SIASA! SIASA! Imekuwa ni wimbo wenye kibwagizo kinachokoleza toka kuanza kwa
mwaka huu wa 2015, hii ni kwa sababu tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu uliopangwa
kufanyika Oktoba mwaka huu.
Hili ni
jambo jema kwa nchi yenye kufuata mfumo wa demokrasia na unaozingatia haki za
watu kuchagua viongozi wanaowataka au kuchaguliwa kuwa viongozi.
Harakati
hizi za uchaguzi zimegeuza akili, nguvu, maarifa na hata mawazo ya watu wengi kiasi
tumesahau kuwekea manani mambo mengine ya msingi na yanayogusa pia maisha yetu
ya kila siku.
Mbali na uchaguzi
mkuu, mwaka huu pia kutakuwa na jambo kubwa na la kimataifa ambao ni Mkutano wa
ishirini na moja (COP21) wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya
Tabianchi (UNFCCC) ambao utafanyika jijini Paris, Ufaransa mwezi disemba mwaka
huu.
Heka heka
unazoziona kwenye kampeni za wagombea kujinadi na kutoa ahadi watakazowafanyia
wananchi endapo watapewa dhamana ya kuwaongoza ziko pia kwenye mchakato wa
kuelekea kwenye mkutano huo wa Paris mwaka huu.
Utofauti wa
mambo haya mawili ni kwamba ahadi za uchaguzi zinaitwa KAMPENI lakini za COP21
zenyewe zinaitwa INDCs. Umewahi kusikia kuhusu INDCs? Ni mchango wa kila nchi katika juhudi za
dunia za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi (Intended Nationally Determined
Contributions – INDCs)
Kwenye
Mkutano wa ishirini wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi
huko Lima, Peru ambapo Tanzania pia ilishiriki, yalifanyika makubaliano ya kila
nchi kuandaa na kuwasilisha maeneo maalumu yatakayokuwa ni mchango wa nchi
husika katika juhudi za dunia za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi (INDCs).
Kwa mujibu
wa Ofisi ya Makamu wa Rais, kwa kushirikiana na wadau, Tanzania kwa sasa inafanya
mchanganuo wa maeneo muhimu yatakayokuwa ni mchango wa Tanzania katika juhudi
za dunia za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambapo kazi ya kuandaa INDCs
inatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Oktoba mwaka huu, na kuwasilishwa kwenye
Sekretarieti ya Mkataba.
Ni jambo la
kupongeza kwa Tanzania kuanza mchakato wa INDCs lakini ni muhimu pia kujua
maana na umuhimu wa INDCs na kutafakari kwa kina kama zina faida au madhara
kabla ya kuwasilisha panapohusika.
Mchakato huo
kwa kiasi kidogo sana umewashirikisha wananchi wa Tanzania hasa wale walioko
kwenye sekta zinazoathirika zaidi na mabadiliko ya tabianchi kama vile kilimo,
afya na uvuvi.
Ikumbukwe
kuwa Tanzania ndo kwanza imevumbua gesi na mafuta, je huu ni wakati muafaka wa
kuingia kwenye mkataba huu wa INDCs? Mkataba ambao unaweza kulazimisha nchi changa
kiuchumi kama yetu kupunguza shughuli za kukuza uchumi zenye viashiria vya
kuharibu mazingira.
Je, kuna
ulazima gani wa nchi kuingia kwenye mkataba huu? Serikali yetu imejipangaje
kusimamia na kutekeleza ahadi zitakazokuwa kwenye hiyo INDCs? Yaliyomo kwenye
mkataba huo yanafaida gani kwa jamii? Wadau wameshirikishwa kwa kiasi gani
wakati wa mchakato?
Majibu ya maswali
haya yatatoa mwanga kwa mtanzania wa kawaida, kujua nchi yake inakwenda kuingia
kwenye mkataba kwa manufaa au madhara yapi ili aweze pia kushiriki katika
utekelezaji wake.
Kabla ya Serikali
yetu haijakwenda kushiriki kikamilifu katika majadiliano ili kupata Mkataba
mpya wa mabadiliko ya tabianchi ambao unatarajiwa kupitishwa mjini Paris mwezi
Desemba, 2015, ni lazima itoe majibu yanayojitosheleza, ijitathmin na
kujiridhisha kuwa inauweza wa kutunza ahadi na kuyasimamia iliyoyapanga.
COP21 ni
muhimu sana kwa sababu utashirikisha nchi 196 ambao ni washiriki wa umoja wa
mataifa kote duniani kuhakikisha kuwa shughuli za maendeleo hazisababishi joto
la dunia kuongezeka kwa zaidi ya nyuzijoto mbili (2oC) juu ya kiwango
cha sasa, ili kuepuka madhara ya mabadiliko ya tabianchi kwa binadamu na viumbe
wengine.
Aidha,
Mkataba utatoa fursa kwa nchi ambazo tayari zinaathiriwa na mabadiliko ya tabianchi kupewe fedha, teknolojia na
kujengewa uwezo wa kuhimili mabidiliko ya tabianchi katika nyanja zote.