maelezo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTB Balozi Charles Sanga (kushoto) na
Meja Jenerali mstaafu Gimonge kuhusu njia mbalimbali zinazotumika katika kupanda mlima
Kilimanjaro muda mfupi kabla ya Balozi Sanga kuanza kuongoza msafara wa kupanda mlima
Msafara huu ujulikanao kama Uhuru Expedition ambao ni mahsusi kwa ajili ya kuadhimisha miaka 52 ya uhuru umeratibiwa na kufadhiliwa na Bodi ya Utalii Tanzania umeanza kupanda mlima Kilimanjaro tarehe 6/12/2013 umeanza kupanda mlima Kilimanjaro tarehe 6/12/2013 umeanza kupanda mlima Kilimanjaro tarehe 6/12/2013 kupitia njia ya Marangu na unatarajia kumaliza zoezi hilo tarehe 10/12/2013.
muda mfupi kabla ya kuanza kupanda mlima Kilimanjaro kupitia njia ya Marangu
Msafara huo wenye jumla ya wapandaji mlima saba (7) ambapo kutoka TTB ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Balozi Charles Sanga, Bw. Musa Kopwe na Bw. Hillary Mushi. Aidha katika msafara huo yumo pia Meja Jenerali mstaafu Gimonge, Bley Mayo, Bibi Lidya Kayuni na Bw. Joan Mwamlima wote kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
expedition wakichanja mbuga kuelekea kituo cha Mandara.
Hii ni mara ya pili kwa Bodi ya Utalii Tanzania kuratibu msafara huu kwa lengo la kuadhimisha siku ya uhuru wa Tanzania Bara. Mara ya kwanza kwa TTB kufadhili Uhuru Expedtion ilikuwa ni mwaka jana ambapo pamoja na TTB Kampuni nyingine kama ya bia ya Serengeti ilijitoleza pia kudhamini Msafara huo wa Uhuru ulioongozwa na aliyekuwa mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Jenerali mstaafu George Waitara.