Picha: Athari za uharibifu wa mazingira

Ng'ombe na mbuzi wakiwa wamesongamana chini ya mti pekee uliokuwepo  katika eneo lililopo  karibu na Shule ya sekondari ya Oljoro  mk... thumbnail 1 summary
Ng'ombe na mbuzi wakiwa wamesongamana chini ya mti pekee uliokuwepo  katika eneo lililopo  karibu na Shule ya sekondari ya Oljoro  mkoani Arusha wakifuata kivuli ili kujikinga na jua Desemba 17, 2016.  Uharibifu wa mazingira unaosabishwa na  shughuli za binadamu  hasa ukataji miti hovyo unaathiri hata viumbe wengine kama picha inavyoonyesha.
Wananchi wakiwa wamebeba bango lenye maneno yanayoeleza  suala la uharibifu wa mazingira kuwa ni tatizo kwao katika mkutano uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye  kijiji cha Ondenderet, Arusha Desemba 17, 2016. 
Mwendesha pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda akiwa amejipumzisha katika eneo lililoathiriwa na uharibifu wa mazingira unaofanywa na binadamu  katika kijiji cha Ormapinu, Arusha Desemba 17, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)