'AL-Qaeeda ilianzisha moto msituni'

Afisaa mkuu mtendaji wa shirika la ujasusi la Urusi, FSB, Alexander Bortnikov... thumbnail 1 summary
Afisaa mkuu mtendaji wa shirika la ujasusi la Urusi, FSB, Alexander Bortnikov, amesema kuwa moto uliozuka katika misitu na kusambaa hadi Kusini mwa bara Uropa na Balkans msimu wa joto, ulianzishwa na kundi la Al Qaeda.
Bwana Alexander aliyasema hayo kwenye mkutano wa kimataifa kuhusu ulinzi mjini Moscow na kuonya kuwa watu walitumia mitandao inayomilikiwa na watu wenye siasa kali, kutuma habari kuhusu maeneo ya kuanzishia moto huo na ambavyo wataweza kuficha ushahidi.
Ingawa wanamazingira pamoja na makundi ya kutetea misitu, wanasema kuwa hakuna dalili kuwa moto huo ulianzishwa na makundi ya kigaidi.
Chanzo: BBC